• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA LAANZA RASMI SIKONGE

Imewekwa: October 7th, 2019

ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA LAANZA RASMI WILAYANI SIKONGE


Afisa Mwandikishaji jimbo la Sikonge, Martha Luleka atoa mafunzo kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata leo katika ukumbi wa Chuo cha Ufundi (FDC). "...nawapongeza kwanza kwa kupata nafasi hii muhimu pia nawaomba muwe karibu na wananchi wakati wa zoezi hili ili kumfanya aweze kutoa taarifa zilizosahihi za mpiga Kura na kuziingiza katika mfumo." Alisema Afisa Mwandikishaji Jimbo.


Mafunzo yalianza kwa maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata kwa kula kiapo cha kujitoa kuwa mwanachama wa chama cha siasa na kiapo cha kutunza siri mbele ya Hakimu, Mheshimiwa Amando Nyami.


Mafunzo haya yanayoratibiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni muendelezo wa mafunzo kwa wote watakaoshiriki katika zoezi zima la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la wapiga kura, ambapo tarehe 4 na 5 ya Mwezi Oktoba 2019 yalifanyika mafunzo ngazi ya Mkoa.


Afisa mwandikishaji Msaidizi jimbo la Sikonge, bwana Edward Mwamotela kwa niaba ya Afisa Mwandikishaji jimbo  alifungua mafunzo haya kwa kusoma hotuba ya ufunguzi ya mafunzo na kuwakaribisha maafisa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Cecilia Kisaka na Steven Nyoka ambao wameshiriki katika kuratibu mafunzo haya ngazi ya Jimbo.


Pia, bwana Mwamotela aliwasisitiza maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata kushiriki kikamilifu katika mafunzo haya ili wakatekeleze zoezi hili kwa umakini na ufanisi, pia alisisitiza katika utunzaji wa vifaa vyote vitakavyohusika katika zoezi hili.


Lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la wapiga Kura linafanikiwa kwa kiwango kikubwa ili kuwa na taarifa sahihi za wapiga Kura.


Katika zoezi hili, wataandikishwa wapiga kura wapya, kwa maana ambao hawakupata nafasi ya kujiandikisha mwaka 2015, ambao wametimiza miaka 18 au watakao kuwa na umri wa miaka 18 ifikapo 2020, pia watapatiwa vitambulisho vipya kwa waliopoteza au kuharibika vitambulisho vya awali na watafutwa kwenye Daftari wale ambao wamepoteza sifa za kuwa wapiga Kura.


Aidha, mafunzo ya siku mbili yatafanyika pia kwa Waandishi Wasaidizi na _BVR Kit Operator_  tarehe 11 na 12 Oktoba 2019, ambao watahusika moja kwa moja katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la wapiga kura ambalo litafanyiaka kwa muda wa wiki moja kuanzia tarehe 14 hadi 20 Oktoba 2019.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa