• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

ZAIDI YA TSH. BILIONI 2 ZIMETUMIKA KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO SIKONGE KWA KIPINDI CHA ROBO YA KWANZA 2024/2025.

Imewekwa: November 6th, 2024

Kamati ya Fedha, Uongozi, na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, imetembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika kipindi cha robo ya kwanza cha mwaka wa fedha 2024/2025, kuanzia Julai hadi Septemba.

Ziara hiyo imelenga kutathmini utekelezaji wa miradi ya ujenzi na ukarabati inayolenga kuboresha huduma za elimu na afya kwa wananchi wa Sikonge. Miradi inayotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa madarasa manne, mabweni mawili, matundu kumi ya vyoo, na nyumba ya mwalimu mbili kwa moja katika Shule ya Sekondari Sikonge, kwa jumla ya Tsh. 508,000,000, ambapo utekelezaji umefikia asilimia 30.

Kamati hiyo imekagua pia ukarabati wa majengo sita katika Hospitali ya Wilaya ya Sikonge, Mlogolo, kwa Tsh. 100,000,000, ambapo utekelezaji umefikia asilimia 50. Miradi mingine ni ujenzi wa shule mpya ya amali ya mkoa inayojengwa katika kijiji cha Mlogolo kwa Tsh. 1,600,000,000, utekelezaji umefikia asilimia 30; umaliziaji wa ofisi ya kata ya Mkolye kwa Tsh. 10,000,000, ambapo ujenzi umefikia asilimia 80; ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Msingi Buriani kwa Tsh. 60,000,000, ambayo ujenzi wake  umekamilika kwa asilimia 100; na ukamilishaji wa zahanati ya Ibaya kwa Tsh. 50,000,000, ambapo utekelezaji umefikia asilimia 70.

Kwa jumla, miradi sita iliyokaguliwa ina thamani ya Tsh. 2,328,000,000, na inatarajia kuboresha huduma za elimu na afya katika wilaya ya Sikonge. Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango imeeleza kuridhishwa kwake na utekelezaji wa miradi hii, ambayo inaendelea kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya kijamii. Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, Mhe. Lwamabano, ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo kwa wilaya ya Sikonge.

Mhe. Lwamabano amempongeza pia Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Sikonge Ndg. Selemani Pandawe kwa usimamizi mzuri wa miradi hii na kueleza kuwa thamani ya fedha zinazotumika inaonekana wazi kupitia maendeleo haya. Miradi hii ni ishara ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuleta maendeleo endelevu na kuboresha huduma za kijamii, hususan katika sekta za elimu na afya, ambazo ni nguzo muhimu katika kuinua ustawi wa wananchi wa Sikonge na Tanzania kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA SIKONGE YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOPENDEKEZWA KUPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 13, 2025
  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa