• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WANAFUNZI WA KIKE WILAYANI SIKONGE WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

Imewekwa: November 23rd, 2025


Na, Edigar  Nkilabo – SikongeDC


Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Bi.Kalista Maina ametoa rai kwa wazazi na walezi wilayani Sikonge kuungana kwa pamoja na kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha Wanafunzi wa kike kusoma masomo ya Sayansi ili kuwa na wastani mzuri wa Wanasayansi wa kike nchini ambao wataendana na kasi ya maendeleo ya teknolojia katika kuihudumia jamii na taifa kwa ujumla.

Bi.Maina ametoa rai hiyo katika Ukumbi wa Samia Hall uliyopo shule ya Sekondari Kamagi wakati wa mafunzo ya kuwezesha mwanaume na mwanamke kushiriki kikamilifu kukuza elimu ya Sayansi kwa Wanafunzi wa kike.

“Rai yangu kwa wazazi na walezi tuungane kwa pamoja kupiga vita ujinga kwa watoto wetu wa kike, mtoto wa kike akitiwa moyo akifundishwa na kthaminiwa anaweza kufanya vizuri kwenye masmo ya sayansi hivyo kwa pamoja tupinge hii hali ili tuwe na Wanasayansi wazuri watakaojenga familia bora na kulitumikia taifa kwa weledi”alisema.

Naye Mratibu wa mafunzo hayo Mwl.Benjamin Mshandete amewataka Maafisa Elimu,Wenyeviti wa Bodi za shule na Wakuu wa shule kwenda kuhamasisha watoto wa kike kupenda masomo ya Sayansi na kuachana na dhana ya kuwa Masomo ya Sayansi ni magumu na kuwaachia Wanafunzi wa kiume.

“Wakuu wa shule na Walimu wa Sayansi fanyeni ziara ya kubadilishana ubunifu kati ya vilabu vya Sayansi kwa pamoja mpeane mbinu za kuwawezesha Wanafunzi wa kike kufanya vizuri kwenye masomo ya Sayansi” aliongeza Mwl.Mshandete.

Kwa upande wake Afisa Tarafa Bi.Faraja Hebel akizungmza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Wilaya amesema Walimu wakitoka kwenye mafunzo wakawaulize Wanafunzi wa kike wanapata changamoto gani wanaposoma masomo ya Sayansi na majibu yao yatasaidia Walimu kuja na mbinu nzuri za kuwafundisha watoto.

Aidha Bi.Faraja amewashauri Walimu wa Sayansi kuwa na utaratibu wa kuwaalika Wanawake waliosoma Sayansi na kufanikiwa ili wawe wanafika shuleni na kuongea na Wanafunzi wa kike hii itawaongezea hamasa na kusoma kwa bidii.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF na kuhudhuriwa na Wenyeviti wa Bodi za shule,Wakuu wa shule na Walimun wa Sayansi.

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KIKE WILAYANI SIKONGE WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

    November 23, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE AHIMIZA UWAJIBIKAJI

    November 20, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA AFYA TARAFA YA KIWERE

    November 17, 2025
  • WAKUU WA DIVISHENI, VITENGO NA MAAFISA BAJETI WATAKIWA KUZINGATIA MPANGO MKAKATI WA HALMASHAURI WAKATI WA UANDAAJI WA BAJETI.

    November 13, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa