• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE AHIMIZA UWAJIBIKAJI

Imewekwa: November 20th, 2025


 

Na,  Edigar Nkilabo SikongeDC

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Mwl.Selemani Pandawe amewataka Wakuu wa Divisheni na Vitengo kutimiza wajibu wao kwa kutafuta namna sahihi ya kuwasaidia wananchi kupitia sekta zao ili kutimiza lengo la serikali la kutoa huduma bora na endelevu kwa wananchi.

Akizungumza katika Ukumbi wa Halmashauri wakati wa kikao cha Kamati ya lishe ya Halmashauri, Mwl. Pandawe amesema ni wajibu wa watendaji kutafuta majawabu ya changamaoto za Wananchi likiwemo suala la upatikanaji wa chakula shuleni wakati wote.

“Tunahitaji kushirikiana wakati wa kutimiza majukumu yetu, lazima tuje na mkakati wa kuhakikisha watoto wote wanapata chakula wanapokuwa shuleni maana kitendo cha baadhi ya watoto kutokula chakula kinaweza kutengeneza matabaka hivyo tuwabaini na kupata jawabu sahihi la changamoto hiyo”alisema.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji amewapongeza wataalamu wa kilimo kwa kuzingatia ushauri wa kamati ya lishe ya Halmashauri kwa kupeleka mashamba darasa kwa taasisi za serikali hasa shule ambapo pembejeo za ruzuku zinazotolewa na Halmashauri zitawanufaisha wanafunzi pindi watakaposimamiwa vyema katika kilimo na kuzalisha kwa tija”aliongeza Mwl.Pandawe.

Kwa upande wake Afisa lishe wa Wilaya Raymond Joseph amesema kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2025/2026, kumekuwa na kuongezeka kwa hali ya utoaji wa chakula kwa wanafunzi wawapo shuleni.

“Ukiangalia takwimu kwa robo hii idadi ya wanafunzi wanaopata chakula shuleni imeongezeka kutoka 95.6% kwa robo ya nne 2024/2025 na kuweza kufikia 96.23% kwa robo ya kwanza ya mwaka 2025/2026 na hata utekelezaji wa siku ya afya na lishe ya kijiji imetekelezwa kwa 100% ” alisema Bw.Joseph.

Naye Mratibu wa wilaya wa Mradi wa BRIGHT kutoka shirika la Nutrition International kwa kushirikiana na Shirika la Engeder health na TAWLA Bi.Khadija Kalipeni ametoa wito kwa kamati ya lishe ya Halmashauri kuwatumia wadau mbalimbali kuchangia chakula cha watoto wawapo shuleni badala ya kupambana na wazazi peke yao.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, jumla ya kaya 11,846 zenye watoto chini ya miaka 5 na wajawazito zimetembelewa na kupewa elimu ya lishe kupitia wahudumu wa Afya ngazi ya jamii kwa kipindi cha Julai hadi septemba, 2025.

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KIKE WILAYANI SIKONGE WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

    November 23, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE AHIMIZA UWAJIBIKAJI

    November 20, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA AFYA TARAFA YA KIWERE

    November 17, 2025
  • WAKUU WA DIVISHENI, VITENGO NA MAAFISA BAJETI WATAKIWA KUZINGATIA MPANGO MKAKATI WA HALMASHAURI WAKATI WA UANDAAJI WA BAJETI.

    November 13, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa