• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WALIMU KUWA MSTARI WA MBELE SHUGHULI ZA MAENDELEO

Imewekwa: July 21st, 2019

WALIMU KUWA MSTARI WA MBELE SHUGHULI ZA MAENDELEO

Walimu waaswa kuwa mstari wa mbele na kushirikiana na jamii kwenye shughuli za maendeleo.

Hayo yalisemwa na katibu wa CCM Wilaya ya Sikonge Bi. Magdalena Daniel alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Shirikisho la Walimu ambao ni wananchama wa CCM Wilayani Sikonge alipokaribishwa kutoa salamu za chama kwa wanashirikisho hao waliokuwa na mkutano wa ndani mapema hivi leo ambapo aliwataka walimu kutumia taaluma yao kuinufaisha Nchi sanjari na kujitoa kwa moyo wa uzalendo wanapohitajika katika shughuli za maendeleo.

Mkutano huo pia ulishirikisha viongozi mbalimbali ngazi ya Wilaya akiwemo Mhe. Joseph Kakunda ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Sikonge, Mhe. Peter Nzalalila ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na wajumbe na viongozi wa Shirikisho hilo ngazi ya Wilaya na walifanikiwa kuzungumza na kutoa maoni mbalimbali yenye tija ya kujenga nchi ya Tanzania.

Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ilikuwa ni umuhimu wa Nembo ya Taifa ambapo  Mhe. Kakunda aliwataka walimu hao ambao ni wanashirikisho kuwafundisha wanafunzi kuijua Nembo ya Taifa na kuilinda kwani ina maana kubwa kwa kila Mtanzania.

Akiongezea hoja hiyo Mhe. Nzalalila aliwataka wanashirikisho kufanya kazi pasipo na majivuno huku akiwahakikishia watumishi wote kuwa Serikali ina mpango mzuri na maslai yao hivyo walimu walio katika shirikisho wawe mfano wa kuigwa katika jamii kwa kuhakikisha majukumu waliyopangiwa yanafanikiwa kwa kiwango cha juu na huko ndio kukitumikia Chama Cha Mapinduzi kwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015 ambayo pia ililenga kuboresha sekta ya Elimu.

Walimu wa Shirikisho wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wenye uhitaji maalumu wanaosoma shule ya msingi Sikonge Maalum mapema walipotembelea shuleni hapo.

Akipokea maelekezo hayo kwa niaba ya wajumbe Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Wilayani Sikonge, Mfaume Zahoro aliahidi kuyazingatia yote yaliyoagizwa huku akisema kuwa wanafanya kazi vizuri kwa kushirikiana na Ofisi ya Afisa Elimu (W) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Martha Luleka huku akihakikisha kuwa matokeo bora kwa wanafunzi ni jitihada za walimu katika kuunga mkono juhudi za Mhe. John Pombe Magufuli ambaye ameboresha miundombinu ya elimu na kutoa elimu bure kwa wanafunzi.

Awali kabla ya kuanza kwa mkutano huo wanashirikisho pia walishiriki katika usafi wa mazingira, hii ikiwa ni agizo la Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Sikonge, Martha Luleka aliyewataka watumishi wote pamoja na wananchi kushiriki kuuweka mji wa Sikonge safi. Tayari utaratibu umewekwa wa kufanya usafi wa maeneo yote kila ifikapo siku ya jumamosi na Wakuu wa Idara na Vitengo wamepangiwa maeneo ya kusimamia na kukagua.

Baada ya Mkutano huo pia wanashirikisho walipata nafasi ya kutembelea shule ya Sekondari Kamagi na kushiriki shuguli za umwagaji wa zege, sambamba na kuongea na wanafunzi wa kidato cha tano ambao wamechaguliwa kwa awamu ya kwanza mwaka huu tangu kuanzishwa kwa shule hiyo.

Imeandaliwa na Kitengo cha TEHAMA Sikonge

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa