• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

UJENZI HOSPITALI YA WILAYA KUKAMILIKA NDANI YA MWEZI MMOJA

Imewekwa: June 26th, 2019

SIKONGE - UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA KUKAMILIKA NDANI YA MWEZI MMOJA.

NA EVELINA ODEMBA

HALMASHAURI ya Wilaya ya  Sikonge yaagizwa kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ndani ya mwezi mmoja .

Agizo ilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Agrey Mwanri alipotembelea ujenzi wa mradi huo na kukuta ukiwa katika hatua mbalimbali ikiwemo hatua ya uezekaji paa kwa baadhi ya majengo wakati majengo mengine yakiwa katikaa hatua ya upigwaji lipu.

Akiwa wilayani hapo Mhe. Mwanri alisema jitihada za dhati zitumike kuhakikisha ujenzi unakamilika ndani ya siku alizoagiza ambapo alitembelea mradi huo tarehe 26 mwezi wa 6 mwaka 2019 kusema kuwa hadi kufikia ataehe 26 mwezi wa 7 mwaka 2019 majengo hayo yawe yamekamilika na kukabidhiwa hivyo alitaka kufungwa kwa umeme wa jenereta ili kuruhusu mafundi kufanya kazi usiku na mchana ili kukimbizana na muda.

Ujenzi huo unategemea kutumia bilioni 1.5 hadi kukamilika kwake, pesa ambazo zimetolewa na Serikali ya awamu ya tano chini ya raisi Joseph Magufuli kwa ajili ya ujenzi wa majengo saba ya awali ambapo ndani ya majengo hayo ni Jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la kufulia, jengo la mionzi, jengo na mama na mtoto, jengo la maabala, jengo la dawa pamoja na jengo la utawala.

Mkuu wa Mkoa Mhe. Agrey Mwanri aliyevaa shati jeupe, Mkuu wa Wilaya Mhe. Peres Magiri mwenye suti nyeusi na Mkurugenzi Mtendaji Martha Luleka pamoja na wataalamu wakitoka kukagua jengo la mama na mtoto katika ujenzi wa hospitali ya Wilaya Sikonge.

Aidha aliagiza kukatwa kwa mishahara ya wajumbe kamati ya mapokezi ya vifaa vya ujenzi wa hospitali hiyo ambao pia ni watumishi wa Halmashauri kutokana na kuwepo kwa madai ya baadhi ya vifaa vilivyonunuliwa kutotosheleza mahitaji. Hivyo alitaka kuundwe tume ya kuchunguzwa madai hayo na ikionekana kuna tatizo watumishi hao wakatwe mishahara yao ili kufidishia mapungufu hayo

Sanjari na hayo pia aliitaka kampuni iliyopewa jukumu la kulinda vifaa vya ujenzi wa hospitali hiyo kuchukuliwa hatua mara moja kutokana na kuwepo kwa wizi wa baadhi ya vifaa ikiwemo nondo 90.

“kampuni hiyo ilipe fidia ya upotevu wa mali hizo na ichukuliwe hatua mara moja, hii haiwezi kuwa hasara ya Halmashauri ni lazima sheria zifuatwe” alisema.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Marha Luleka alipokea maelekezo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi kama ilivyoagizwa huku akishukuru kuongezewa kwa muda huo kuwa kutawezesha kazi kukamilika kwa vizuri. Sanjari na hayo pia aliwashukuru wadau mbalimbali wa maendeleo Sikonge ambao wameweza kujitolea kufanikisha ujenzi wa Hospitali hiyo ikiwa ni njia ya kuunga mkono serikali ya Awamu ya Tano.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa