• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

“TWENDENI TUKASIMAMIE KWA USHIRIKIANO MKUBWA WATOTO WAPATE CHAKULA SHULENI” MHE. CHACHA.

Imewekwa: January 31st, 2024

Na. Robert Magaka – Sikonge.

Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe Wilaya ya Sikonge Mhe. Simon Chacha ametoa wito kwa Watendaji wa Kata Wilaya ya Sikonge Kwenda kusimamia upatikanaji wa chakula shuleni leo katika kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe ngazi ya kata na Wilaya katika kipindi cha robo ya pili,Oktoba hadi Desemba 2023 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri.

Mhe. Chacha ameongeza kuwa ni lazima watendaji kutumia mbinu zote na rasilimali zinazopatikana katika maeneo yao ya kiutendaji kuwezesha upatikanaji wa  lishe bora shuleni.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Ndg. Seleman Pandawe ametoa rai kwa wataalam kuhakikisha wanaishirikisha jamii kikamilifu katika suala zima la uchangiaji wa chakula shuleni ili Watoto waendelee kupata lishe bora shuleni.

Naye Afisa Lishe Wilaya ya Sikonge Bi. Veronica Ferdinand amesema katika robo ya pili utoaji wa chakula shuleni ndio kiashiria pekee ambacho kimeonesha udhaifu katika utekelezaji wake katika kata zote za wilaya ya Sikonge.

Aidha Bi. Ferdinand ameongeza kuwa katika robo hii ya pili Oktoba hadi Desemba yapo mambo mazuri yaliyoonekana wazi ikiwemo kupanda kwa kiashiria cha utekelezaji wa siku ya Afya na Lishe ya Kijiji kutoka 71% (Julai hadi Septemba, 2023) hadi kufikia 98% (Oktoba hadi Desemba, 2023). Vile vile jumla ya miche 500 ya kisasa ya miti ya miembe imepandwa katika shule kumi za Msingi katika Wilaya ya Sikonge ikiwa na lengo la kuboresha lishe shuleni.

Akihitimisha kikao hicho Mhe. Chacha amepongeza kwa juhudi zinazoendelea ili kuboresha lishe katika ngazi ya kata na Halmashauri kwa ujumla, imebainika kuwa kati ya viashiria 10 katika kadi alama za lishe ni viwili tu ndio vipo katika rangi ya njano na nane vilivyobaki vipo katika rangi ya kijani ambayo ni kiashiria cha kufanya vizuri katika utekelezaji wa afua za lishe.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

    June 14, 2025
  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

    June 06, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa