• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA UMEME WA JUA UNAONUFAISHA KAYA ZAIDI YA 190 WILAYANI SIKONGE

Imewekwa: September 5th, 2019

SIKONGE-  KAYA ZAIDI YA 195 ZANUFAIKA NA UMEME WA JUA ULIOZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU 2019

Na Richard Mrusha na Evelina Odemba

WANANCHI wa Kijiji cha Mgambo kilichopo Kata kitunda Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora wamesema kuwa kupata umeme kumeongeza fursa ya ajira katika kijiji hicho.

Umeme huo umetekelezwa na kampuni ya Power Corner kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliogharimu zaidi ya bilioni moja umeunganisha kaya zaidi ya 195 zilizopo katani hapo.

Akitoa taarifa wakati wa Ufunguzi wa mradi huo Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Mhe. Peres Magiri alisema kuwa hivi sasa Kata ya Kitunda inafurahia huduma hiyo ya umeme wa jua na kwani umewezesha vijana kujiajiri kwa kujishughulisha na mambo mbalimbali ya uzalishaji ili waweze kujiinua kiuchumi.

Naye kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mzee Mkongea Ali wakati wa kuzindua mradi huo unaotumia umeme wa jua aliwataka wazalishaji hao kufuata bei elekezi kwa wateja wao ili wananchi wote wanufaike na mradi huo, aliongeza kuwa mpango wa Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inapeleka Umeme ndani ya Vijiji vyote ili wananchi waweze kufungua viwanda vidogo vidogo kwani nchi inaendeshwa kwa sera ya viwanda.

Akizungumza kwaniaba ya Wananchi wenzake Muuzaji wa  Maji na Soda, alisema wanaipongeza sana Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya Power Corner ambao ndio watekelezaji wa mradi kwani hivi sasa wanakunywa maji baridi, nyama safi ambazo zinahifadhiwa kwenye friji, ukilinganisha na awali.

Pia alisema mradi huo wameupokea kwa mikono miwili na kwakweli hawakutegemea kulingana na historia yake kwani awali walikuwa wanatumia umeme wa sola ya kawaida za kufunga wenyewe ambao pia ulikuwa hauna nguvu kama ulivyo huo uliozinduliwa na Mwenge wa Uhuru.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Mkongea Ali akizindua Umeme wa Jua Power Corner ulioko kata ya kitunda Wilayani Sikonge.

"Nataka niwaeleze ndugu waandishi wa Habari leo vijana wetu wanatengeneza Simu hapahapa pindi zinapoharibika,wachomeleaji wamerahisishiwa,saluni zinafunguliwa kwakweli mambo mazuri sana." Alisema Anthon Lukas.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Sikonge Martha Luleka alisema kuwa ujio wa Umeme katani hapo umeongeza chachu kwa wananchi kuweza kufanya kazi lakini pia umeimarisha usalama katika makazi ya watu ukilinganisha na huko nyuma.

Akizungumza kwa niaba ya Madiwani, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Sikonge Mhe. Peter Nzalalila alisema kuwa Wananchi wa Kata ya Kitunda wameitumia vyema fursa hiyo kujiwezesha kiuchumi jambo linalosaidia kuongeza mapato katika Halmashauri yake. “Kipindi cha nyuma walikuwa wanafunga safari Mpaka Sikonge mjini kilomita nyingi kutoka hapa, kwa ajili ya huduma za kuchomelea n.k lakini leo hii shughuli hizi zinafanyika hapahapa kijijini kwao, ni jambo la kushukuru” alisema.

Naye Meneja Mradi Kanda ya Tabora Kutoka Kampuni hiyo ya Power Corner Erick Moshi akizungumzia mradi huo alisema Kampuni imepata ushirikiano mkubwa Kutoka mamlaka za Serikali katika kung'amua vijiji stahiki vya kupata huduma ya umeme.

Alisema kuwa mradi huo uliazishwa rasmi mwanzoni mwa mwezi Machi 2018 ambao unauwezo wa kuzalisha kilo-whatts 20 kwa kijiji cha Mgambo na umeme wenye uwezo kilo-whatts 28 kwa vijini vya Mkola na Mwenge.

Kwaupande wake kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Mzee Ali akizungumzia mradi, kwanza alipongeza Serikali kwa kuweka Mazingira wezeshi kwa Kampuni ya Power Corner na kufikia hatua ya kuwapatia umeme wananchi.

"Nawaomba ndugu zangu wa Kijiji hiki cha Mgambo muweze kuulinda mradi huu ambao naamini umeleta fursa kubwa kwenu katika kuongeza uzalishaji Mali na kujiongezea kipato." Alisema Ali.

Alisema kuwa mradi ni mzuri na kwakuwa ameridhishwa na kiwango cha ujenzi wake na Fedha ilitotumika hivyo ameuzindua rasmi kupitia Mwenge wa Uhuru 2019.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa