• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MHE. DKT. GWAJIMA AIPONGEZA SIKONGE KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

Imewekwa: December 21st, 2024

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, ameipongeza Wilaya ya Sikonge kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo. Pongezi hizo amezitoa leo alipokuwa akikagua miradi ya ujenzi wa madarasa matatu katika Shule ya Msingi Ukanga na madarasa matatu katika Shule ya Msingi Batilda. Miradi hii inajengwa kwa fedha za mapato ya ndani pamoja na fedha kutoka Serikali Kuu, ambapo jumla ya shilingi milioni 120 zimetumika.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo, Mhe. Gwajima amepongeza uongozi wa wilaya ya Sikonge kwa kufanya kazi kwa umoja na kusikilizana kati ya chama na serikali , jambo ambalo limechochea maendeleo katika wilaya hiyo na kuifanya iendelee mbele bila vikwazo. Amesisitiza kuwa ushirikiano wa viongozi wa chama na serikali ni muhimu katika kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa mafanikio.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Mhe. Cornel Lucas Magembe, amemuomba Mhe. Gwajima msaada wa kuimarisha mapambano dhidi ya mila na desturi kandamizi zinazochelewesha maendeleo, hususan katika sekta ya elimu. Mhe. Magembe ametaja mchezo wa Chagulaga, unaoshamiri zaidi katika jamii ya wafugaji wilayani Sikonge, kama moja ya mila inayosababisha ndoa za utotoni na kukatisha masomo ya watoto wa kike, hasa wa jamii ya Kisukuma.

Ziara ya Mhe. Gwajima imehitimishwa kwa kuweka mawe ya msingi katika ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Ukanga na Shule ya Msingi Batilda. Akihutubia wananchi baada ya zoezi hilo, Mhe. Gwajima amewaomba wananchi  kuwa mstari wa mbele katika kupinga mila na desturi zinazokwamisha jitihada za serikali za kuwaletea maendeleo. Ametoa wito kwa wanaume mashujaa kuwa mabalozi wema wa mabadiliko, ili kuelimisha jamii kuhusu mila na desturi zinazozuia maendeleo, hususan mchezo wa Chagulaga.

 Mhe. Gwajima amewakumbusha wananchi  kuwa Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imekuwa ikiwekeza kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya mkoa wa Tabora. Kwa mfano, Serikali imetumia jumla ya shilingi trilioni 1.1 kwa mkoa wa Tabora pekee katika miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa bilioni 186.6 kwa sekta ya elimu, bilioni 37.5 kwa sekta ya afya, bilioni 199.6 kwa sekta ya maji, bilioni 12.3 kwa ajili ya ruzuku ya pembejeo za kilimo, na bilioni 302.4 kwa ajili ya sekta ya nishati,bilioni 281.6 kwa ajili ya sekta ya miundombinu ya barabara na shilingi bilioni 52 kwa ajili ya sekta ya umwagiliaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa