• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

KAMPENI YA FUKUA FUKUA YATUA RASMI SIKONGE

Imewekwa: September 10th, 2019

KAMPENI YA FUKUA FUKUA YATUA RASMI SIKONGE

Na Evelina Odemba

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Agrey Mwanri aendesha kampeni ya fukua fukua Wilayani Sikonge ili kuwabaini wahalifu waliojificha Wilayani hapa.

Kampeni hii iliyoanzishwa rasmi Mkoani Tabora na kutangazwa Wilayani hapa  kupitia mkutano wa hadhara, ilijikita kushirikisha wananchi katika utekelezaji  kwa kuwataka kuandika majina ya wahalifu wanaowatambua na kuyakabidhi kwa Kamanda wa Polisi Wilaya, huku akiwataka kuendelea kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi mara watakapoona mtu wasiyemfahamu au wanayemtilia mashaka katika maeneo wanayoishi.

Akifafanua kuhusu kampeni hiyo Mhe. Mwanri ambaye aliambatana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji (W), alisema kuwa zoezi hili litasimamiwa na kuratibiwa na jeshi la polisi wakati wa kuendesha msako wa kuwafukua wahalifu kokote walipojificha kwa kuwashirikisha wananchi  kwasababu wao ndio wapo katika maeneo hayo na ni rahisi kupata taarifa kwa haraka.

Aidha alitahadharisha kuwa kila msako utakapoendeshwa basi Polisi wawepo ili kutoa muongozo na taratibu kisheria, huku akionya kuwa hatoruhusu wananchi kujiendea wenyewe kuwakamata wahalifu kwa sababu hataki mtu aonewe, kubugudhiwa wala kufanyiwa vitu vya ajabu.

“Kama una habari yeyote muhimu tunakuomba utoe taarifa kwa jeshi letu la Polisi,wao watalifanyia kazi kwa weledi tunajua kuwa wahalifu wote wanaokuja hapa lazima wana mawakala wao mahali hapa, wacha tuitwe wanoko lakini mahali hapa pabaki salama” alisema.“Hatutakubali wahalifu watoke kokote walipotoka na kuona kuwa Tabora ni sehemu pekee wanayoweza kukaa kwa amani huku wakiendelea kutekeleza uhalifu wao” aliongeza huku akisisitiza kuwa watu wote wafanye kazi muda wa kazi na si kushinda kwenye nyumba za starehe muda wa asubuhi.

Akiongea na wananchi baada ya zoezi la kuandika majina ya wahalifu kwa siri kufanyika kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Barnabas Mwakarukwa aliwataka wale wote walioandikwa majina yao kujisalimisha kituo Kikuu cha polisi kilicho karibu naye haraka iwezekanavyo kabla hawajasakwa kokote walipo.“Tuna mtaji mkubwa sana wa wananchi ambao sio wahalifu, wahalifu ni wachache na mtandao wao unafahamika, kwani wanatoka miongoni mwa jamii” alisema.

Naye mkuu wa wilaya ya Sikonge Mhe. Peres Magiri alisema kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu Wilayani hapa kwani Serikali imejipanga vizuri kiutekelezaji. Hivyo wananchi wawe na amani katika utekelezaji wa majukumu yao ya kiuchumi.“tunahitaji kuendeleza amani na utulivu katika maeneo yetu, hatuwezi kufanya vizuri katika maswala ya biashara na uwekezaji kama hatuna amani na watu wetu hawawezi kufanya biashara zao wakiwa huru bila hofu”

Alihitimisha kwa kuagiza majina ya wale wote waliosomwa wakihusishwa na uhalifu kuhakikisha kuwa wameripoti katika vituo vya polisi kabla ya saa 12 jioni siku hiyo waliyotajwa majina kabla msako haujapita kokote.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa