• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE INAVYOIISHI KWA VITENDO KAULI YA “MTEJA NI MFALME” KWA KUTOA ELIMU NA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

Imewekwa: October 7th, 2025

Na, Anastazia  Maguha – Sikonge.


Ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja Kitaifa mwaka huu , Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge imeadhimisha wiki hiyo kwa kumulika huduma mbalimbali zinazotolewa kwa Wananchi huku ikibeba kaulimbiu ya Huduma bora na endelevu kwa kila Mwananchi INAWEZEKANA.

Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kupitia kitengo muhimu cha Afya katika Hospitali ya Wilaya – Mlogolo wameadhimisha wikii ya Huduma kwa mteja kwa kutoa elimu na kuwasihi Wananchi wa wilaya ya Sikonge na waliopo karibu kufika katika Hospitali hiyo kwa ajili ya vipimo na kupatiwa matibabu pindi  wanapobainika kuwa na changamoto za kiafya.

“Tumejipanga vizuri tunatoa vipimo vya magonjwa ya Selimundu ( Sickle cell), Homoni (hormones) , huduma ya Mama na Mtoto lakini pia magonjwa yasiyoambukizwa mfano. Presha na Kisukari na huduma za dharula ( emergency) zote zinapatikana hivyo akija mgonjwa atatukuta tuko tayari kumpatia huduma stahiki na atafurahi”alisema Muuguzi, Rose Mgita.

Kwa upande wake Mtaalam wa maabara, Elkana Paul alisema kwasasa serikali imeboresha huduma kwa kununua vifaa vya kisasa ambavyo vimesaidia na kuwezesha huduma za uchunguzi wa magonjwa mbalimbali.

“Maabara yetu inahudumia wananchi wote wa ndani na nje ya Sikonge, huduma za vipimo tunazotoa ni vipimo vya ini,figo,homoni, mkojo na malaria hivyo wiki hii ya huduma kwa mteja tunawakaribisha wananchi wote kwani mtaji wa kwanza wa mwanadamu ni afya” alisema Elibariki Paul.

Kwingineko, Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji nayo ilianza maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja kwa kuwatembelea wateja na kutoa elimu ya biashara, sheria za ulipaji kodi pamoja na utoaji wa leseni za biashara kidijitali.

Kaimu Mkuu wa Divisheni hiyo, Princelous Hunja alisema lengo lao ni kuhakikisha mfanyabiashara  wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge anapata huduma bora na endelevu hasa kipindi hiki cha maendeleo ya sayansi na teknolojia ambapo huduma nyingi zinatolewa kidijitali.

“Wiki hii wateja wetu waitumie kwa kujifunza na kuzifahamu taratibu zote za upatikanaji wa huduma zetu, na sisi tuko tayari kuwahudumia muda wote kama kuna sehemu hawaelewi wasikae kimya waulize maswali tutawapa majawabu sahihi”alisema.  

"Tunawakaribisha Wafanyabiashara wote katika Ofisi zetu zilizopo hapa Halmashauri, kwa ajili ya kupata huduma na elimu mbalimbali juu ya ulipaji kodi na kupata leseni Kidigitali,lakini msisite kutoa maoni na ushauri ili kuboresha huduma hizi ili kwa pamoja tuweze kuleta tija na ustawi wa Halmashauri yetu na Taifa kwa ujumla”aliongeza.

Kaulimbiu ni Huduma Bora na Endelevu kwa Kila Mwananchi Inawezekana.

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA SIKONGE SEKONDARI KUANZA KUFUNDISHWA TEHAMA KWA VITENDO

    November 25, 2025
  • WANAFUNZI WA KIKE WILAYANI SIKONGE WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

    November 23, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE AHIMIZA UWAJIBIKAJI

    November 20, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA AFYA TARAFA YA KIWERE

    November 17, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa