• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MIRADI 20 YAKAGULIWA NA KAMATI YA WATAALAMU (CMT) ROBO YA KWANZA KWA MWAKA WA FEDHA WA 2025/2026

Imewekwa: October 12th, 2025


 

Na, Edigar Nkilabo – Sikonge DC

Kamati ya Wataalamu(CMT) ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri (Mwenyekiti) imefanya ziara katika kata mbalimbali na kukagua miradi ishirini (20) ya elimu, afya na vikundi vya mkopo vya Wananwake vinavyonufaika na mkopo wa Halmashauri wa asilimia kumi unaotokana na mapato ya ndani.

Katika ziara hiyo kamati imeridhishwa na kupongeza utekelezwaji wa baadhi ya miradi ya elimu na afya na miradi mingine ikionekana kusuasua kukamilika kutokana na usimamizi mbovu wa waliopewa dhamana ya kusimamia miradi hiyo na msisitizo wa  kamati zaidi ukiwa kwenye uundaji wa kamati za mapokezi, manunuzi na ujenzi unaozingatia mwongozo na taratibu za ujenzi wa mfumo wa kuendesha miradi kwa kutumia nguvu kazi na vifaa vya serikali (Force Account).

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo kwa niaba ya Kamati ya Wataalamu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ndugu Selemani Pandawe amesema baadhi ya miradi imekwama kutokana na usimamizi mbovu wa wenye miradi hasa pale unapogundua wamekiunka utaratibu wa kuunda kamati za ujenzi,manunuzi na mapokezi.

“Hakikisheni mnazingatia miongozo ya force account haiwezekani Mtendaji wa Kijiji unakuwa Mwenyekiti wa Kamati sasa ukiwa sehemu ya watekelezaji wa mradi ni nani atakayefuatilia maendeleo ya mradi huo na kubaini mapungufu yanayotokea. Mfano hapa Ipole mradi wa matundu 25 ya vyoo umekwama na fedha ipo kutokana na usimamizi mbovu na kamati zenyewe hazieleweki jamani hizi ni fedha za serikali zitumike kwa kufuata utaratibu unaotolewa na serikali”alisema Pandawe.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji amewasimamisha kazi Watumishi wawili ambao ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ipole na Mtendaji wa Kijiji cha Ipole kwa kushindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo na kupelekea kukwama kwa mradi wa ujenzi wa matundu 25 ya vyoo wenye thamani ya shilingi milioni Sitini na Nane unaotokana na fedha za SWASH.

Kwaupande wao baadhi ya Wajumbe akiwemo Katibu Tawala wa Wilaya ya Sikonge wamewapongeza wasimamizi wa miradi ambao wamefanya vyema kwa kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyoendana na thamani ya fedha

“Tuwapongeze kwa kusimamia fedha za mradi kwa weledi na uadilifu hata kuukamilisha mradi huu kwa viwango stahiki, sasa watu wa Ipole wakija hapa watakuwa salama kwa kwakuwa taka zote zitachomwa pia watanawa mikono yao na kuwa salama”alisema Katibu Tawala Ndugu Andrea Ng’hwani.

“Kwakweli baadhi ya wasimamizi wa miradi wako vizuri wanajua nini wanafanya na kamati zao za ujenzi zimeundwa kwa kufuata taratibu na miongozo hivyo ninaamini hizi milioni 250 za ujenzi wa kituo cha Afya Kiloleli zitasimamiwa vyema tukija hapa tutakuta mradi unaenda kwa kasi” alisema Seif Salum Mjumbe wa Kamati.

Naye Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Ipole Dkt.Justina Joseph akisoma taarifa ya kichomea taka na kinawia mikono chenye thamani ya shilingi milioni ishirini (20) amesema ujenzi wa kichomea taka utasaidia kuondoa uchafu na kutunza mazingira.

Kwaupande wake Afisa Manunuzi ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Wataalamu wa Halmashauri amewataka wasimamizi wa miradi kufuata utaratibu wa manunuzi kwa kuhakikisha kamati zote zinatimiza wajibu wake na kutunza nyaraka zote.

“Nyaraka zote za manunuzi zitunzwe ili wakaguzi wanapokuja wakute kila kitu kipo sawa na jambo la mwisho nawasisitiza wanakamti mnatimiza wajibu wenu kulingana na jukumu la kamati husika ili kazi ziende msitegeane”alisema Nibwene Mwaikandage Afisa Manunuzi.

Ziara hiyo ya siku mbili imehitimishwa kwa kukagua miradi ishirini inayotekelezwa katika Kata mbalimbali za Halmashauri ya wilaya ya Sikonge, yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni Moja na Milioni Mianne(Bil.1.4)

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA SIKONGE SEKONDARI KUANZA KUFUNDISHWA TEHAMA KWA VITENDO

    November 25, 2025
  • WANAFUNZI WA KIKE WILAYANI SIKONGE WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

    November 23, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE AHIMIZA UWAJIBIKAJI

    November 20, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA AFYA TARAFA YA KIWERE

    November 17, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa