• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

KAMATI YA SIASA YA WILAYA IMEKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYANI SIKONGE.

Imewekwa: January 16th, 2025

Na, Edigar Nkilabo

Kamati ya siasa ya wilaya ya Sikonge imekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa katika kata za Igigwa na Sikonge ikiwemo miradi ya elimu ,barabara na maji ikiwa ni sehemu ya ukaguzi wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2020.

Akizungumza katika ziara hiyo kwa niaba ya mwenyekiti wa CCM Wilaya , Katibu wa CCM wilaya ya Sikonge SALUM MGAYA amesema ameridhishwa na usimamizi wa miradi ya elimu unaofanywa na makatibu wa kamati za ujenzi na wataalamu wa halmashauri katika shule za sekondari Sikonge na Usupilo.

“Kamati ya siasa ya wilaya tumeridhishwa na kazi inayofanywa na mafundi katika kikubwa ongezeni kasi ya ujenzi ili miradi hii ikamilike kwa wakati kama ambavyo mmeeleza katika taarifa zenu ili watoto waanze kunufaika na miradi kwa kupata elimu bora”alisema.

Kwa upande wake mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Sikonge , katibu tawala wa wilaya ya Sikonge Andrea Nghw'ani amesema serikali itafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na kamati ya siasa ili kuboresha huduma kwa wananchi pamoja na  kuwapunguzia watoto adha ya kutembea umbali mrefu kufuata elimu huku makatibu wa kamati za ujenzi wa shule za sekondari Sikonge na Usupilo wanaelezea faida walizopata wananchi wa maeneo hayo ikiwemo ajira.

“Wananchi wengi wamejitokeza na kuomba kazi mbalimbali katika miradi hii na hata vibarua wanaofanya kazi hapa ni vijana wa humu humu Sikonge wamejipatia kipato kupitia miradi hii”

Baada ya kuipa kisogo miradi ya elimu macho yalielekezwa katika miradi ya Barabara ikiwemo ujenzi wa mitaro katika barabara za Sikonge ambapo Meneja wa TARURA wilaya ya Sikonge Elgidius Method amesema bajeti ya wilaya ya Sikonge kwa mwaka huu wa fedha ni zaidi ya milioni mia tano ambapo fedha hizo zimetumika katika ufunguzi wa Barabara,uchongaji na ukarabati wa Barabara pamoja na kuweka taa katika baadhi ya vitongoji hasa vile ambavyo tayari Barabara zake zimejengwa kwa kiwango cha lami.

Ziara ya kamati ya siasa ya wilaya ya Sikonge imehitimishwa kwa kukagua mradi wa maji katika kijiji cha Wankolongo ambapo baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa  wameelekeza kilio chao kwa mafundi wanaotekeleza mradi huo ambao wanaonekana kusuasua licha ya kuwa nje ya muda wa mkataba wa kukamilisha mradi huo.

“Mradi huu hauendi kwa kasi kwasababu fedha za mradi huu tulihamishia kwenye mradi mwingine ambao ulikuwa unatekelezwa kwa kasi lakini tayari tumeomba fedha nyingine zikija tunarejesha kwenye mradi huu ili uweze kukamilika na kuwatua kina mama ndoo kichwani kama serikali inavyosisitiza”Mhandisi Fikiri Samadi Meneja RUWASA Sikonge.

Mradi huo wa maji unagharimu zaidi ya shilingi milioni mia tisa na unatarajia kunufaisha wakazi zaidi ya elfu nane.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa