• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU, WAFANYIKA WILAYANI SIKONGE.

Imewekwa: May 20th, 2021


MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU, WAFANYIKA WILAYANI SIKONGE.

Tarehe 20.5.2021

Na.Anna Kapama.

Ni mkutano wa Baraza la Madiwani ambao hufanyika kila baada ya miezi mitatu(robo) ambao hukutana na kujadili taarifa mbalimbali za maendeleo na utekelezaji wa miradi kila robo mwaka.

Akifungua Mkutano huo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe.Rashid Magope amesema katika mwaka wa fedha 2020/2021, Halmashauri ilipanga kukusanya mapato ya ndani Shilingi Bilioni 3 lakini mpaka robo hii ya tatu wamefanikiwa kukusanya Shilingi Bilioni 1.3 tu. Hivyo amewaagiza ofisi ya Mkurugenzi na watumishi wote kuongeza juhudi zaidi Katika  kusimamia ukusanyaji wa  mapato kwa kutumia vifaa vya kielekroniki.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Tabora, Siame Mathias akitoa salamu kutoka ofisi ya Katibu Tawala mkoa amesema kuwa watumishi wanapaswa  kuzingatia sheria za Utawala bora na kushirikiana kwa wote ili kuhakikisha haki sawa na uwazi kwa wananchi kwa manufaa bora na ujenzi wa Taifa. Madiwani ikiwa hawaridhishwi na utendandaji wa mtumishi katika Halmashauri kufuata  Sheria na hatua za kinidhamu na si kumkataa moja kwa moja pasipo kufuata taratibu zilizowekwa.

Aidha,Siame amewataka wananchi kuchangamkia fursa ya uwekezaji kwa kuwekeza hasa katika kilimo cha Korosho ambacho kitaleta tija kwa wananchi hao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sikonge,Mhe.Peres Magiri amewataka madiwani kushirikiana na watendaji na watumishi kwa ukaribu katika ukusanyaji wa mapato,huku akiwasisitiza wananchi kushiriki katika suala la ulinzi na usalama kwa kutoa taarifa za uhalifu kwa vyombo vya ulinzi na usalama.

Mhe.Magiri amewataka wawekezaji kuja kuwekeza Sikonge kwa kuwa ni miongoni mwa maeneo ambayo fursa za uwekezaji wa shughuli za  kiuchumi zinapatikana ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa  mashamba makubwa(block farming),maeneo ya kuwekeza viwanda ambayo yametengwa na Halmashauri.

Katika suala la mbio za Mwenge wa Uhuru ambao unatarajiwa kupokelewa julai 13, 2021Mkoani Tabora,Mhe.Magiri amewataka watumishi na wananchi kushirikiana kufanikisha mbio za Mwenge wa Uhuru kama ambavyo imekuwa ikifanya wakati wote kwa kuwa Sikonge imekuwa ikiongoza katika mkoa wa Tabora.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Sikonge, Anna Chambala amewasisitiza watumishi na viongozi wote wa Halmashauri kuchapa kazi na kutenda haki na usawa katika kutoa huduma kwa wakazi wa  Wilaya ya Sikonge ili kutimiza ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mkutano huu wa Baraza la Madiwani umehudhuriwa na wajumbe mbalimbali ikiwa ni pamoja na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Tabora,Mkuu wa Wilaya, wakuu wa Idara mbalimbali,Waheshimiwa madiwani,viongozi wa Chama cha mapinduzi(CCM) na baadhi ya wakazi wa wilaya ya Sikonge.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa