• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI SIKONGE LAPITISHA BAJETI YA MWAKA 2021/2022

Imewekwa: February 2nd, 2021

BARAZA LA MADIWANI SIKONGE LAPITISHA BAJETI YA MWAKA 2021/2022

NA ANNA KAPAMA
2 February 2021


BARAZA la Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge limepokea na kupitisha makisio ya bajeti ya mwaka wa fedha wa 2021/22 ya shilingi bilioni 28.3. Mkutano wa Baraza hilo ulifanyika katika ukumbi wa chuo cha Ufundi na Maendeleo (FDC) na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Wilaya

Katika baraza hilo lililoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Rashid Magope ambae alisema kuwa bajeti ya mwaka ujao imepanda kwa asilimia 11.7 ukilinganisha na bajeti ya mwaka wa fedha wa 2020/21 ya shilingi bilioni 25.3.

Aidha, bajeti hiyo imejikita katika vipaumbele vya kukuza uchumi na maendeleo ya viwanda, kuimarisha miundombinu ya elimu, afya, kujenga skimu za umwagiliaji wa kilimo cha mpunga katika bonde la Kalupale,uanzishaji wa mashamba makubwa ya kilimo cha mazao ya kudumu kama vile miembe na korosho,kukamilisha sehemu ya jengo la Utawala la Halmashauri, ujenzi wa viwanda vidogo na kutatua kero za wananchi.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Mhe. Peres Magiri amewataka wananchi kujiandaa na kuchangamkia fursa kutokaana na kuanzishwa kwa kiwanda cha kati cha kuchakata mazao ya nyuki pamoja na kilimo cha mashamba makubwa.

Pia aliongeza kuwa bajeti ijayo ni vema ikajikita katika uimarishaji wa kilimo cha mashamba makubwa ambayo yataweza kuzalisha mazao mengi na kupelekea kupata fedha nyingi ili asilimia 10 ya fedha hizo ikatumika kuwezesha vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu pamoja na kuchangia miradi ya maendeleo kwa kiwango kikubwa.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka Madiwani kushirikiana na watendaji na jamii katika kuhamasisha wanafunzi wa madarasa ya mitihani kuweka kambi za maandalizi ya mitihani ya kitaifa ili kuinua ufaulu.Alisema hatua hii inakwenda sanjari na mapambano dhidi ya utoro sugu miongoni mwa wananfunzi ikiwemo kuwachukulia hatua wahusika kwa mujibu wa Sheria zilizopo. Pia alimuagiza Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Sikonge kuendesha oparesheni ya kukamata wanafunzi wote watakaokutwa wakicheza kamari na mabonanza.  

Nae Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Sikonge, Tito Luchagula aliwashukuru wajumbe wa baraza wakiwemo Madiwani na Wataalam waliohusika katika mchakato wa kuandaa na kujadili bajeti hiyo lakini pia aliwashukuru wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo kwa kuhudhuria baraza hilo na kupitisha bajeti hiyo.  

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa