• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WAGONJWA ZAIDI YA 400 WAMEPATIWA MATIBABU YA KIBINGWA WILAYANI SIKONGE

Imewekwa: October 3rd, 2025



Na, Anastazia Maguha


Wananchi zaidi ya 400 wilayani Sikonge wamenufaika kwa matibabu mbalimbali  ya kibingwa kupitia programu ya Madaktari Bingwa wa Rais Dkt.Samia, ambapo kambi ya Madaktari Bingwa wa aina sita na Muuguzi mbobezi wa chumba cha upasuaji imetoa huduma kwa wananchi hao kwa muda wa siku tano.

Daktari Bingwa wa Watoto na kiongozi wa timu ya Madaktari hao Dkt.Lyimo Michael amesema zoezi la utoaji wa matibabu limefanikiwa kwakiasi kikubwa kwakuwa wananchi wengi wamehamasika na kujitokeza kwa wingi katika Hospitali ya Wilaya na kupatiwa matibabu stahiki.

“Ndani ya hizi siku tano tumefanikiwa kuona wagonjwa zaidi ya 400, robo tatu ni wagonjwa wan je wapatao 250 na 150 ni wagonjwa waliolazwa”alisema Dkt.Lyimo.

“Magonjwa yanayoongoza kwa Watoto ni selimundu(sickle cell) na malaria kali inayosababisha kuharibika kwa figo pamoja na maambukizi ya bakteria kwa watoto wachanga na kwaupande wa upasuaji wananwake wanachangamoto ya vimbe kwenye via vya uzazi(Ovarian cisty) na Henia kwa wanaume”aliongeza.

Aidha Dkt.Lyimo amesema magonjwa ya ndani yaliyoonekana kuongoza ni presha,vidonda vya tumbo na homa yabisi ambapo wataalamu wamehakikisha wanawahudumia wagonjwa wote waliopatikana na changamoto ya magonjwa hayo.

Naye Mocha Shimba ambaye ni mkazi wa kata ya Mpombwe ameushukuru uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Sikonge na Rais Dkt.Samia kwa kusogeza huduma za matibabu ya kibingwa kwani wananchi wengi wamenufaika nan huduma hizo kwa gharama nafuu.

“Nimefika hapa na mwanangu anaumwa nimepokelewa vizuri amefanyiwa matibabu na kupatiwa dawa kwa gharama ndogo tofauti na kufuata huduma hizo kwenye hospitali za rufaa”alisema.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Sikonge  Dkt.Catherine Katisho  amesema huduma hizo za kibingwa zimeenda sambamba na kuwajengea uwezo wataalamu wa afya wa Hospitali ya Wilaya.

“Wananchi wetu wamepata huduma lakini nitoe wito kwa wananchi kujitokeza tangu siku ya kwanza ili kupata huduma kwa wakati na kunufaika na huduma hizi za kibingwa kwa gharama nafuu”Dkt.Katisho.

Matibabu hayo ya kib ingwa  yalianza kutolewa tarehe 29/09/2025 na kufikia tamati tarehe 03/10/2025.

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MIRADI 20 YAKAGULIWA NA KAMATI YA WATAALAMU (CMT) ROBO YA KWANZA KWA MWAKA WA FEDHA WA 2025/2026

    October 12, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE INAVYOIISHI KWA VITENDO KAULI YA “MTEJA NI MFALME” KWA KUTOA ELIMU NA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    October 07, 2025
  • WAGONJWA ZAIDI YA 400 WAMEPATIWA MATIBABU YA KIBINGWA WILAYANI SIKONGE

    October 03, 2025
  • MAMBO SHWARI KWA KIDATO CHA TANO NA SITA SHULE YA SEKONDARI SIKONGE

    September 22, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa