• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

Imewekwa: June 25th, 2025


Na, Edigar Nkilabo 


Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, imeendesha mafunzo maalum ya mfumo wa E-Utendaji(PEPMIS) kwa wasimamizi wa watumishi wa umma ili kuimarisha uwajibikaji na utendaji wa watumishi wa umma kwa kutumia mfumo huo wa kisasa.

Akizungumza katika ukumbi wa Halmashauri wakati akiwasilisha mada juu ya mfumo huo, Mwezeshaji Mfumo wa PEPMIS kutoka OR-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi.Cecilia Meela amesema kuwa mafunzo hayo ni utekelezaji wa adhima ya serikali ya kuimarisha utekelezaji wa majukumu kwa njia ya kidigitali unaoendana na kasi ya mabadiliko sayansi na teknolojia.

“Mafunzo haya yanalenga kuelekezana juu ya matumizi sahihi ya mfumo mzima wa e-Utendaji katika uwekaji wa taarifa za utekelezaji hasa kipengele cha tathmini ya utendaji wa watumishi.Ni wajibu wa watumishi wote kuhakikisha tunaujua huu mfumo asiwepo yeyote anayeachwa nyuma ili iwe rahisi kuweka utekelezaji na kuidhinisha kwakuwa upandishaji wa madaraja unategemea taarifa za utendaji za kwenye mfumo wa PEPMIS na si vinginevyo”alisema Bi.Meela.

Aidha Bi.Meela amewataka watumishi kuwa makini na taarifa zao kwa kutunza nywila za akaunti zao za PEPMIS kwakuwa wapo baadhi ya watu si waaminifu wanaweza kuzitumia vibaya taarifa hizo na kumletea hasara mtumishi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Sikonge Ndugu Andrea Ng’hwani amewataka Watendaji wa Kata,Wakuu wa Shule za Sekondari,Walimu wakuu wa Shule za Msingi,Waganga Wafawidhi wa Vituo vya Afya, Zahanati na Wakuu wa Idara na vitengo wote kuzingatia mafunzo hayo ili yalete tija kama ilivyokusudiwa.

“Mkitoka hapa mkatekeleze mafunzo mliyopatiwa najua hata zile changamoto za awali zitapatiwa suluhisho kupitia mafunzo haya, hakikisheni na wale waliokosa hii fursa mnawaelekeza”alisisitiza Ng’hwani.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Dkt.Christopher Nyalu ameishukuru OR-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kutoa mafunzo hayo ambayo yataongeza weledi na ufanisi kwa watumishi wa umma katika utekelezaji wa majukumu katika mfumo wa e-Utendaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

    June 14, 2025
  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

    June 06, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa