• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WATUMISHI AJIRA MPYA SIKONGE WAASWA KUWA WAADILIFU.

Imewekwa: October 7th, 2022

Sikonge_Tabora

Watumishi wapya wa Idara ya Afya waliopangiwa kazi katika Vituo mbalimbali vya kutoa huduma za Afya Wilaya ya Sikonge wametakiwa kuzingatia sheria, na miongozo iliyowekwa na kufanya kazi kwa uadilifu.


Hayo yameelezwa katika kikao kilichofanyika Hospitali ya Wilaya ya Sikonge na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kwa ajili ya kutoa Elimu kwa watumishi hao.


Awali akifungua kikao hicho Mganga Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Dkt.Christopher Nyalu amewasisitiza watumishi hao kuwa waadilifu  wakizingatia sheria na taratibu kwa za utendaji kazi huku wakiwaasa kuwa na Mahusiano mazuri mahali pa kazi.


Aidha, Dkt.Nyalu amewataka watoa huduma za Afya kuwa waaminifu katika ukusanyaji wa Mapato yatokanayo na utoaji wa huduma za Afya ili Serikali iweze  kupata Mapato yatakayosaidia kuendeleza huduma kwa Wananchi.


"Kila Mtu humu ni Mkusanya mapato, Serikali inaingiza Mapato kupitia huduma zinazotolewa, hivyo ni vyema kuzingatia taratibu zilizowekwa za ukusanyaji wa Mapato"Dkt.Nyalu.


Kwa Upande wake Katibu wa Afya Hospitali ya  Wilaya ya Sikonge Masoud Ally amewasisitiza kutoa huduma zilizo bora kwa wateja ili kuendelea kulinda sifa njema ya taasisi husika.


"Unapofanya jambo baya hautatajwa wewe Jina lako, ila taasisi unayofanyia kazi "  Amefafanua zaidi 


Sambamba na Hilo Mganga Mfawidhi wa  Hospitali teule ya Wilaya ya Sikonge Dkt.Peter Songolo amewataka watumishi hao kutunza vyema Raslimali zilizo katika maeneo yao ya kazi .


Ofisi ya Mkurugenzi kupitia Idara Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe imetoa mafunzo elekezi  kwa waajiriwa wapya wa Sekta ya Afya wakiwemo Madaktari na Wauguzi ambao wamepangiwa vituo vya kazi  katika Hospitali na vituo vya Afya Wilaya ya Sikonge lengo ikiwa kuwajengea uwezo wawapo katika maeneo yao ya kitolea huduma.


#kaziiendelee

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa