• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WATENDAJI KATA WAPEWA SEMINA SIKONGE

Imewekwa: December 29th, 2018


WATENDAJI KATA WAPEWA SEMINA SIKONGE

Wananchi waaswa kusherekea sikukuu ya mwaka mpya kwa amani na utulivu bila kuvunja sheria za nchi, ili kuhakikisha usalama kwa kila raia.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa wilaya ya Sikonge mkoani Tabora Mhe. Peres Magiri katika semina kufunga mwaka 2018 iliyoandaliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Sikonge Bi. Martha Luleka alipokuwa akizungumza na watendaji wa kata na kuwasisitiza kuyapeleka kwa wananchi wanaowaongoza.

Semina hiyo ililenga kuwawezesha watendaji wa kata kujua majukumu yao na kuyatekeleza ipasavyo ili kujenga Sikonge yenye maendeleo ilitolewa na  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi. Martha Luleka akishirikiana na baadhi ya wakuu wa idara na vitengo, pamoja na kuu ya wilaya ikiongozwa na DC Mhe. Peres Magiri.

Bi. Martha alitoa somo la ujasiliamali kwa watendaji kama njia mojawapo ya njia ya kuwapatia kipato na kuongeza ukusanyaji wa mapato kwenye kata zao. Pia walitakiwa kubuni miradi itakayoleta kipato mfano mazao na hata kutumia simu zao kujifunza mambo mbali mbali ya kimaendeleo. Akitoa msisitizo alisema “kiongozi anaanzia nyumbani kwake, ili uwe kiongozi wa pekee lazima ufanye kitu cha kipekee”.

Akizungumza na watendaji Mhe. Peres  amepiga marufuku kumbi za video kufanya maonesho usiku huku watoto wakiwemo ndani ya kumbi hizo, kwani jambo hilo ni kinyume cha sheria na pia wakati mwingi picha zinazooneshwa usiku katika kumbi hizo ni zile zisizo na maadili. Hivyo kuwataka watendaji wa kata kushirikiana na vyombo vya usalama kukomesha jambo hilo.

Miongoni mwa mambo aliyoyakemea Mhe. Magiri ilikuwa ni pamoja na watoto kushiriki katika mchezo wa bahati nasibu maharufu kama KUBET, kucheza Puli muda wa kazi pamoja na kufanya mikusanyiko isiyokuwa na kibali kutoka katika vyombo vinavyohusika.

Watendaji hao pia walipewa rai kuhakikisha wanatenda haki kwa wananchi wanowaongoza kwani kutokufanya hivyo ni kusababisha wananchi waichukie serikali yao, na kuongeza kuwa serikali ya awamu ya tano ni sikivu na inawajali wananchi wake wote.

Kwenye swala la kilimo mkuu wa wilaya alisisitiza wakulima kupiga dawa mapema  kwenye mazao  ili kuepukana na wadudu waharibifu ambao wamekuwa wakishambulia mazao yaliyoko shambani, pia wakulima na wafugaji watengewe maeneo maalumu ili kuepuka migogoro ya ardhi.

Wafugaji wamesisitizwa kupitisha mifugo yao kwenye njia zilizotengwa maalumu kwa ajili ya mifugo. kwani kupitisha mifugo  kwenye barabara kuu ni kuharibu hifadhi ya barabara wakati serikali inatumia pesa nyingi kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma bora za barabara. Hivyo wafugaji wanaokiuka kanuni hiyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Magiri pia alizungumzia swala la elimu katika wilaya ya Sikonge na kusema kuwa inatakiwa vyumba 7 vya madarasa kuongezwa ili kukabiliana na changamoto ya watoto 361 ambapo wavulana walikuwa 126 na wasichana 235 walikosa kuchaguliwa baada ya vyumba vya madarasa kuwa vichache.

Swala la mimba mashuleni ambalo ni changamoto, awamu hii Mhe. Magiri amelivalia njuga na kusema kuwa “hatokubali kila siku watoto wanapigwa mimba na sisi tupo tunaangali tu.’’ Hivyo kila mtu ajiandae kuanzia ngazi ya familia na Watendaji watoe ripoti mapema ya kesi za mimba kwa jeshi la polisi ili zishugulikiwe mapema na sio kungojea hadi wanafunzi wanajifungua.

Watendaji hao kwa pamoja walitoa ahadi ya kuyafanyia kazi maagizo waliyopewa wao kama viongozi katika kata zao watatoa maamuzi kwa haki na kutatua changamoto ambazo zilikuwa sugu mwaka 2018. Ili kutekeleza sera Mhe. Raisi kuelekea kwenye uchumi wa viwanda.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa