• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WASISITIZWA KUZINGATIA SHERIA,KANUNI NA MIONGOZO INAYOTOLEWA NA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI

Imewekwa: August 4th, 2025

Na Edigar Nkilabo

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Sikonge Mwl.Benjamin Mshandete amewataka Wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata kuhakikisha wanazingatia viapo vyao kwa kutunza siri na kusimamia katiba, sheria ,kanuni na miongozo inayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi kipindi cha Uchaguzi Mkuu.

Mwl.Mshandete  ametoa kauli hiyo katika ukumbi wa Halmashauri wakati akifungua mafunzo ya Wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata.

“Hakikisheni viapo mlivyokula mnavizingatia pia someni katiba ya nchi, pitieni sheria,kanuni na miongozo inayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na pale ambapo mtu hujaelewa basi uliza ili ufafanuliwe  ili mkafanye kazi vizuri katika maeneo yenu wakati wa Uchaguzi mkuu kwa niaba ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi” alisema.

Aidha Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Sikonge amewapongeza Wasimamizi wasaidizi wote walioaminiwa na kuteuliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na kuwakumbusha kuwa uteuzi wao umezingatia bidii, utendaji kazi, weledi na uzalendo wao kwa Taifa hivyo hawana budi kuwajibika ipasavyo kama walivyoaminiwa na tume.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mafunzo Bi.Fatuma Said amemshukuru Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Sikonge kwa kuwapa somo ambapo amesema kupitia mafunzo haya wataenda kufanya kazi kwa umahili na ufanisi.

“Kwakweli katika kundi letu hili wapo baadhi ya Wasimamizi wasaidizi ambao hii ndiyo mara yao ya kwanza kusimamia uchaguzi na wengine wanauzoefu hivyo tukishirikiana kwa pamoja na haya mafunzo tuliyopatiwa basi tutafanya vizuri katika maeneo yetu”alisema.

Wasimamizi wasaidizi (40) kutoka kata zote (20) za Jimbo la Uchaguzi la Sikonge wanashiriki mafunzo hayo ya siku tatu ikiwa ni maandalizi kuelekea kutekeleza majukumu kama Wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata  katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.   

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MIRADI 20 YAKAGULIWA NA KAMATI YA WATAALAMU (CMT) ROBO YA KWANZA KWA MWAKA WA FEDHA WA 2025/2026

    October 12, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE INAVYOIISHI KWA VITENDO KAULI YA “MTEJA NI MFALME” KWA KUTOA ELIMU NA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    October 07, 2025
  • WAGONJWA ZAIDI YA 400 WAMEPATIWA MATIBABU YA KIBINGWA WILAYANI SIKONGE

    October 03, 2025
  • MAMBO SHWARI KWA KIDATO CHA TANO NA SITA SHULE YA SEKONDARI SIKONGE

    September 22, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa