• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WANATEMBEA KM.9 KUFUATA ELIMU

Imewekwa: March 28th, 2019

WATEMBEA KM 9 KUFATA ELIMU.

WANAFUNZI wanaokaa kijiji cha Ulilwansimba kilichoko kata ya Misheni Wilayani Sikonge mkoani Tabora,  wanalazimika kutembea  Km 9 kufuata elimu.

Wanafunzi hao wa elimu ya msingi hutembea kuelekea Shule ya YombaKulovya iliyopo umbali wa Km. 4.5 kutoka kitongoji cha Ulilwansimba jambo linalopelekea kiwango cha ufauru kushuka kutokana na umbali huo ukilinganisha na umri mdogo wa wanafunzi hao kuweza kumudu masomo na mwqendo kwa wakati mmoja.

Akizungumzia jitihada za Serikali katika kukabiliana na changamoto hiyo  Diwani wa kata ya Misheni  Mhe. Juma Ikombola alisema kuwa wamepokea jumla ya shilingi Ml 156.6 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa, matundu sita ya vyoo pamoja na nyumba moja ya walimu ijulikanayo kama two in one.

Mh. Ikombola aliongeza kuwa mbali na hayo wanakijiji wa Ulilwansimba pia walishaanza jitihada mapema kwa kujenga shule shikizo ambayo ina madara mawili ambayo ni darasa la awali pamoja na darasa la kwanza na tayari limesajili wanafunzi wa mwaka huu hivyo basi ukamilishwaji wa madarasa yanayofuatia utawaokoa wanafunzi wengi kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kutafuta eleimu.

Sanjari na hilo wanakijiji pia walijitokea kusafisha eneo na kuchimba msingiikiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali katika kuboresha miundombinu ya elimu. Akisisitiza umuhimu wa kujitolea Bi. Clementina Kadiko ambaye ni mtendaji wa kijiji cha Usupilo alisema kuwa wamejipanga kutumia nguvu ya wananchi pamoja na pesa iliyotolea na Serikali ili kupata ongezeko la Ofisi ya walimu pamoja na vyumba vingine vitatu vya madarasa kwani matofali tayari yapo.

Diwani wa kata ya Misheni Mhe. juma akishirikiana na wananchi kusafisha eneo litakalojengwa Shule ya Msingi Ulilwansimba

Akizumgumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya Bi. Faraja alisema kuwa shule ni mali ya kijiji husika hivyo kuwaasa wanakitongoji wa Ulilwansimba kujitolea kwa moyo wote kuhakikisha wanafanikisha ujenzi wa shule hiyo kwa ubora na muda waliopangiwa. Vilevile alitolea mfano swala la wanafunzi kushindwa kwenda shuleni kipindi cha masika kutokana na mito kujaa maji. Bi Faraja alisema kuwa linahepukika iwapo shule itakamilika.

Akitoa shukrani za dhati kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi mwenyekiti wa CCM Kata ya Misheni alisema kuwa ni jitihada za Serikali kuhakikisha wananchi wake wanaboreshewa miundombinu ikiwemo ya Elimu hivyo basi kilichofanyika ni kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

    June 06, 2025
  • WALIMU ZAIDI YA 200 WA SHULE ZA MSINGI WILAYANI SIKONGE WAPEWA MAFUNZO YA KUFUNDISHA SOMO LA KIINGEREZA.

    May 21, 2025
  • CCM, MKOA WA TABORA YAWAHIMIZA WAZAZI NA WALEZI WILAYANI SIKONGE KUCHANGIA CHAKULA SHULENI

    May 19, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa