• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WALIMU WAPYA WALIOAJIRIWA WILAYANI SIKONGE KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2025 WAPATIWA MAFUNZO ELEKEZI YA UTUMISHI WA UMMA.

Imewekwa: July 14th, 2025


Na Edigar Nkilabo


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Ndugu Selemani Pandawe amewataka Walimu kuwa waadilifu na kuzingatia maadili ya Utumishi wa umma pindi wanapotekeleza majukumu yao na kuwa mfano bora wa kuigwa katika jamii.

Akifungua mafunzo elekezi ya Utumishi wa umma kwa Walimu walioajiriwa wilayani Sikonge katika kipindi cha mwaka 2025, katika ukumbi wa Elimu maalumu Pandawe amewataka Walimu kuzingatia ujuzi na elimu watakayopewa na Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) ili waweze kutumia maarifa hayo katika kulea na kuwafundisha watoto kwa uadilifu na weledi.

“Utumishi wa Umma hauna mipaka wakati wote ishi katika uadilifu haijalishi uko ndani au nje ya Ofisi hakikisha unakuwa muadilifu na kuyaishi maadili ya utumishi wa umma.”alisema.

Naye Katibu Msaidizi TSC Wilaya ya Sikonge Bi. Farida Ndyamukama amesema mafunzo haya yanalenga kukazia maadili na uadilifu katika utendaji kazi kama ambavyo serikali inasisitiza mafunzo hayo ili kuepusha masuala ya utovu wa nidhamu kwa walimu.

“Mafunzo haya tunaanza kuyatoa kwa Walimu walioajiriwa baadae tutayafanya kwa Walimu wote kwakuwa wapo walimu ambao wametekwa na mazingira na kujisahau kama wao ni Watumishi wa umma hivyo inabidi kuwapiga msasa ili waendelee kuwa waadilfu katika utendaji wao wa kazi”alisema.

Kwa upande wake Afisa Elimu Kata ya Misheni Mwalimu Leonard Mwimbe amesema mafunzo hayo yataenda kuleta mabadiliko chanya katika Wilaya ya Sikonge na kuongeza ufaulu kwakuwa Walimu watafanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia maadili na miiko ya utumishi wa umma.

“Kwakuwa tayari tumeshakuwa Walimu mahali popote tunapokuwa ni lazima kuishi kama Walimu , pia tujitahidi kutumia rasilimali za umma kwa manufaa ya umma kama ambavyo serikali inakusudia na huo ndiyo uadilifu”alisema.

Kwa mujibu wa takwimu za Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita (2021/2022, 2022/2023 hadi 2023/2024) Walimu wapatao 12,600 kote nchini, walifukuzwa kazi na kupoteza nafasi za utumishi wa umma kwa makosa ya kimaadili na kukosa uadilifu kazini.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WALIMU WAPYA WALIOAJIRIWA WILAYANI SIKONGE KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2025 WAPATIWA MAFUNZO ELEKEZI YA UTUMISHI WA UMMA.

    July 14, 2025
  • Waganga Wakuu wamemtunukia Rais Tuzo, Mhe. Mpango awapongeza, atoa maelekezo mahususi.

    July 13, 2025
  • MKUU WA WILAYA MTEULE WA WILAYA YA SIKONGE MHE.THOMAS MYINGA ALA KIAPO KUANZA KAZI RASMI AKIRITHI MIKOBA YA MTANGULIZI WAKE MHE.CORNEL MAGEMBE

    July 02, 2025
  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa