Na Linah Rwambali
Wenyeviti wa Bodi za shule na Walimu wamepatiwa mafunzo ya kutekeleza program ya uboreshaji wa mazingira katika shule teule kama shule mfano ili kuboresha mazingira ya shule.
Mafunzo hayo ambayo yameanza leo na yanatarijwa kumalizika kesho yanafanyika kwa ufadhili wa Serikali ya Canada kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi na Afisa Elimu Sekondari Bi.Kalista Maina amewataka washiriki kuhakikisha wanaelewa na kufanyia kazi yote watakayofundishwa.
“Shirika la UNICEF linatumia pesa nyingi kuendesha mafunzo haya, nmnatakiwa kuhakikisha mnasikiliza kwa makini na kuyaweka katika vitendo yale yote mtakayojifunza na kusaidia utunzaji wa mazingira katika shule zenu” amesema.
Aidha Maina ameipongeza shule ya Sekondari Kamagi kwa utunzaji mzuri wa mazingira na kuwaomba washiriki wa mafunzo hayo kuiga mfano wa Kamagi.
Naye Mratibu wa Mafunzo (W) Ndugu Benjamin Mshandete amesema baada ya mafunzo hayo zoezi la uboreshaji wa mazingira shule za Sekondari kwa Wilaya ya Sikonge litafanyika katika kumi ambazo zitatumika kufundishia shule zingine namna bora ya kuhifadhi mazingira ya shule.
“Awali zoezi la uboreshaji wa mazingira litafanyika katika shule teule kumi ambazo ni Mole, Kamagi,Tutuo, Kiwele, Kiloli, Usunga, Igigwa, Mibono, Kilumbi na Nyahua ambapo shule hizi zitatumika kama mfano kwa shule zingine” amesema.
Jumla ya Wenyeviti wa bodi za shule kumi na walimu wa mazingira 23 toka shule zote za Sekondari Wilayani Sikonge wamehudhuria mafunzo hayo ambayo yameanza leo na yanatarajiwa kumalizika kesho.
Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC
Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora
Simu: 0767135460
Simu: 0767135460
Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz
Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa