• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WAKUU WA DIVISHENI, VITENGO NA MAAFISA BAJETI WATAKIWA KUZINGATIA MPANGO MKAKATI WA HALMASHAURI WAKATI WA UANDAAJI WA BAJETI.

Imewekwa: November 13th, 2025

Na Edigar  Nkilabo – Sikonge DC

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Sikonge Mwl.Selemani Pandawe amewataka Wakuu wa Divisheni, Vitengo na Maafisa bajeti wote kuzingatia maelekezo yanayotolewa na wataalamu pamoja na mpango mkakati wa Halmashauri ambao utasaidia bajeti zao kuakisi mahitaji halisi ya Halmashauri na serikali kwa ujumla.

Mwl.Pandawe amesema hayo katika ukumbi wa Halmashauri wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa wakuu hao wa divisheni na vitengo pamoja na Maafisa bajeti.

“Mafunzo mnayopatiwa leo mnapaswa kuyazingatia kwa makini maana wakati wa bajeti mnatakiwa kuutumia ujuzi mnaopewa hapa pamoja na maelekezo yote ya wataalamu bila kusahau mpango mkakati wa Halmashauri yetu ya Sikonge ili bajeti zenu ziweze kutekelezeka na kuakisi mahitaji halisi ya Idara na Vitengo vyenu” alisema.

“Mkawashirikishe Watumishi waliopo chini ya Idara na Vitengo vyenu wakati wa uandaaji wa bajeti ili na wao watoe maoni yao, naamini mkifanya hivyo zitaandaliwa bajeti zinazokidhi mahitaji na kutatua changamoto zenu”aliongeza.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Mwl.Pandawe amewataka Wakuu wa Divisheni na Vitengo kukaa pamoja na Watumishi waliopo chini ya Ofisi zao na kubangua bongo ili kuja na vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitasaidia kuongeza mapato ya Halmashauri yatakayowezesha upatikanaji wa huduma bora kwa Wananchi.

Kwaupande wake Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu Ndg.Aidan  Frument amesema maagizo yote yaliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji yatafanyiwa kazi na matokeo chanya yatapatikana kwa kuhakikisha washiriki wote wa mafunzo wanazingatia hayo wakati wa uandaaji wa bajeti.

“Nyote mmesikia haya tunayoelekeza myazingatie ili wakati wa bajeti kusitokee changamoto zaidi tupange kwa kuzingatia mpango mkakati wetu, dira ya taifa pamoja na ilani ya chama tawala hapo tutakuwa ndani ya malengo ya serikali na bajeti zetu zitaendana na mahitaji”alisema Ndg.Frument.  

Mafunzo hayo ya siku mbili yanalenga kujengeana uwezo wa kuandaa mipango na bajeti zinazoendana na mikakati ya Halmashauri pamoja na serikali kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KIKE WILAYANI SIKONGE WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

    November 23, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE AHIMIZA UWAJIBIKAJI

    November 20, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA AFYA TARAFA YA KIWERE

    November 17, 2025
  • WAKUU WA DIVISHENI, VITENGO NA MAAFISA BAJETI WATAKIWA KUZINGATIA MPANGO MKAKATI WA HALMASHAURI WAKATI WA UANDAAJI WA BAJETI.

    November 13, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa