• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WAHESHIMIWA MADIWANI SIKONGE WAPATA MAFUNZO

Imewekwa: November 20th, 2021

WAHESHIMIWA MADIWANI SIKONGE WAPATA MAFUNZO

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, ndugu Seleman Pandawe ameandaa mafunzo kwa waheshimiwa Madiwani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo Cha Maendeleo Sikonge (FDC) kwa siku mbili kuanzia tarehe 19 hadi 20 Novemba 2021.  

Mafunzo hayo yameshirikisha taasisi mbalimbali katika kutoa mafunzo kwa Madiwani na Wakuu wa Idara, wakiwemo TAKUKURU, Mahakama, Polisi, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda, Ofisi ya RAS pamoja na chuo cha Uhazili Tabora.

Akifungua mafunzo hayo Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, amesisitiza umakini na utulivu ili tufaidike na mafunzo hayo muhimu Kwa ajili ya kuendesha Halmashauri yetu kwa kufuata Sheria na taratibu zilizopo.

Akitoa mafunzo Wakili wa Mahakama ya Mwanzo Bi. Winfrida Magai alishauri tupende kujisomea sheria ili kuwa na uelewa kwa baadhi ya mambo na pia kufahamu mabadiliko ya sheria ambayo hutokea. Pia ameeleza taratibu za kufuata pindi unapotaka kufungua kesi pamoja na vitu vinavyohitajika kwenye baadhi kesi mfano kesi za mirathi.

Nae, Mtaalam kutoka Chuo cha Uhazili, ndugu Brevius Ludovic alitoa mafunzo juu ya Kazi, Wajibu na Majukumu ya Diwani pamoja na misingi ya usimamizi wa fedha na taratibu za manunuzi. Pia aligusia kuhusu mbinu za Menejimenti na Uongozi katika Utawala wa kidemokrasia.

Aidha, Mtaalam kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, ndugu Onesmo Msalangi alitoa somo kuhusu uzingatiaji wa kanuni za Maadili ya Waheshimiwa Madiwani ya Mwaka 2000 lakini pia alitoa mafunzo ya dhana ya mgongano wa Maslahi Kwa Madiwani na Viongozi wa Umma.

Mada juu ya Taratibu za Mikutano na uendeshaji wa shughuli za Halmashauri (Vikao na Mikutano) ilitolewa na Afisa Utumishi na Utawala ndugu Nico Kayange akishirikiana na Afisa Sheria ndugu Paschal Kapinga. Nae Mtaalam kutoka TAKUKURU Bi. Ilandike Lucas alitoa Elimu juu ya kuzuia na kupambana na Rushwa halikadhalika Muwakilishi wa OCD Kamanda Isp. Mdoe Waziri alitoa mafunzo juu ya ulinzi na usalama. Na Mtaalam kutoka ofisi ya RAS ndugu Siame Mbati alitoa Mada ya hatua za kinidhamu kwa Watumishi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Mhe. Rashid Magope kwa niaba ya Madiwani wote aliwashukuru wawasilishaji wa Mada zote kwa uwasilishaji mzuri na unaoeleweka. Kwa ujumla mafunzo yalikuwa mazuri na yenye kushirikisha ambapo wajumbe waliweza kuuliza maswali, kujadili na kupata ufafanuzi.

Nae, Mbunge wa Jimbo la Sikonge, Mhe. Joseph Kakunda alipata kushiriki mafunzo na kueleza baadhi ya mambo hasa juu ya Sheria na Taratibu pia aliuliza swali Kwa watoa Mada wote akihoji neno Bahati mbaya huweza kuchunguzwa vipi? akitoa mfano wa stori ya Dereva na Bosi wa sehemu fulani kilichowakuta, swali ambalo lilifafanuliwa vizuri na Mtaalam kutoka ofisi ya OCD na pia Mtaalam wa TAKUKURU.

Aidha, Mhe. Kakunda ambae pia alikuwa mshiriki alipewa nafasi ya kufunga mafunzo hayo na kuchua nafasi kuwashukuru walioandaa mafunzo na kushauri siku nyingine yafanyike kabla ya kuanza mabaraza ili kujinoa juu ya uendeshaji wa shughuli za Halmashauri na usimamizi wa Miradi Kwa ujumla. Aliongeza kwa kusema kuwa wamejifunza juu ya uhusiano wa Serikali na mihimili kama Polisi, Mahakama na TAKUKURU.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa