• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

WAFANYA KAZI KUPANDA MADARAJA

Imewekwa: May 1st, 2019

WAFANYAKAZI KUPANDA MADARAJA.

SERIKALI kuwapandisha daraja wafanyakazi wote wanaostahili kupanda daraja  kwa kuzingatia taratibu na sheria za nchi.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Peres Magiri alipokuwe mgeni rasmi kwenye sherehe za maadhimisho ya sikukuu ya  wafanyakazi Duniani  ambapo wilayani hapa ziliazimishwa katika viwanja vya TASSAF. Pia zilihuzuliwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Sikonge Mhe. Peter Nzalalila pamoja na wafanyakazi wa sekta zote katika Halmashauri ya Sikonge.

Akizungumzia swala la maslai ya watumishi Magiri alisema kuwa serikari imejipanga vizuri kuhakikisha watumishi wote wanaostahili kupanda madaraja wanapandishwa madaraja hayo huku akisisitizia kuhusu watumishi kulipwa madai yao kwa wakati kwani kitendo cha kulimbikiza madai kinaleta dosali katika utendaji kazi. Huku akigusia kuwa watumishi wote wanaohamishwa vituo vyao vya kazi walipwe kwanza garama za kuamishwa na sio kupeleka mtumishi kituo kingine cha kazi bila kumjali ataishi vipi.

Kuhusu swala la rushwa mgeni rasmi alisema kuwa ni marufuku kwa mtu yeyote awe mtumishi au sio mtumishi kujihusisha na swala la rushwa kwani ni adui wa maendeleo huku akiwataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kujituma kwani maendeleo ya Taifa la Tanzania yanategeme uwajibikaji wa kila mwananchi.

Mgeni rasmi Mhe. peres Magiri akisikiliza maelezo kwenye banda la idara ya Kilimo siku ya maazimisho ya mei mosi

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Bi. Martha Luleka alikemea kitendo cha baadhi ya watumishi kuonekana katika nyumba vinakouzwa vilevi muda wa kazi na kusema kuwa yeye kama mwajili hatokubali kutiwa doa na watumishi wote wa namna hiyo. Huku akiongeza kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya watumishi wa namna hiyo  ikiwemo kukabidhiwa hati ya utumishi goigoi ambavyo watakabidhiwa hadharani ili kuwaumbua.

Pamoja na kuwapongeza wafanyakazi waliopo katika Halmashauri yake  Bi. Martha aliongeza kuwa mazingira ya Sikonge bado ni rafiki kwa watumishi kwani yanawawezesha kumudu gharama za maisha kutoka mwezi mmoja hadi mwezi mwingine, huku akiwaasa watumishi wenye jinsia ya kiume kuweka wazi mishahara  kwa wenzi wao ili kusaidia ustawi wa familia kwani kumekuwa na desturi ya wanamme kuficha mapato yao jambo linalokwamisha maendeleo ya familia.

Akitoa pongeze zake kwa niaba ya Madiwani Wilayani Sikonge Mhe. Nzalalila alisema kuwa watumishi wamekuwa mstari wa mbele kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kutoa huduma bora kwa wananchi na kwa wakati huku akiongezea kuwa waendelee kuwa na lugha nzuri kwa wananchi wao na pia wawe na ubunifu katika nafasi walizokabidhiwa.

Sherehe hizo zilipambwa na burudani mbalimbali ikiwemo vikundi vya nyimbo pamoja na maonesho ya kazi za kila idara ambapo katika idara ya maendeleo iliyomtoa mfanyakazi bora Bi. Alice Frank alielezea kuwa wanalengo la kuboresha maisha ya wananchi kwa kutoa mikopo  kwa wanawake, vijana na walemavu ambapo katika hilo mgeni rasmi alisema kuwa ni vizuri kiwango cha mkopo kikaongezwa kwani lengo ni kuwanyanyua wananchi wote na sio wafanyakazi pekee.

Akitoa shukrani zake kwa niaba ya wafanyakazi mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa bwana Nasoro alisema kuwa wanaipongeza serikali kwa kuwajari watumishi huku akiomba malalamiko yote ya watumishi kufanyiwa kazi ikiwemo kupanda madaraja na kulipwa malimbikozo yao kwa wakati.



IMETOLEWA NA KITENGO CHA TEKINOLOJIA HABARI NA MAWASILIANO

SIKONGE

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa