• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

VITAMBULISHO VYAMSUKUMA NDANI MTENDAJI KATA.

Imewekwa: April 17th, 2019

VITAMBULISHO VYAMSUKUMA NDANI MTENDAJI KATA.

MKUU wa Mkoa amuweka ndani Mtendaji wa kata ya Kitunda Bwana Jerad Hamis Kwa tuhuma za kuuza vitambulisho vya wajasiliamali wadogowadogo kwa shilingi elfu 26.

Hatua hiyo ilichukuliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Agrey Mwanri alipozungumza na wananchi kutaka kujua nini kinachokwamisha zoezi la uuzwaji wa vitambulisho hivyo ambapo wajasiliamali hao walilalamikia kuuziwa kwa shilingi elfu 21 mpaka elfu 26.

Mtendaji huyo aliwauzia wakazi wa kitunda Mgodini vitambulisho kwa bei tofauti na bei iliyopangwa na Serikali ambayo iliagiza  kitambulisho kimoja kichangiwe shilingi elfu 20 tu ambazo ni gharama za utengenezaji na si vinginevyo.

Akilaani kitendo hiko Mwanri alisema kuwa hakuna mahali kamati ya ulinzi na usalama ilikaa na kupitisha zaidi ya pesa iliyowekwa na serikali hivyo maagizo ya mtendaji huyo hayajulikani yalipotokea. Aliongeza kuwa pesa zote za ziada zilizotozwa zirudishwe kwa wananchi na Mtendaji huyo awajibishwe, aliongeza kwa kusema “amepoteza sifa ya kuwa mtumishi kwani anaichanganya Kadamnasi”

Pia alitoa maagizo kwa Mkuu wa Wilaya ya Sikonge kufuatilia jambo hilo kwa kwa ukaribu ili haki itendeke na hatua zichukuliwe kwa mujibu wa sheria ya nchi huku akitoa onyo kwa jeshi la Polisi kutoivuruga kesi hiyo kwani ina maslai mapana ya nchi ya Tanzania.

Akipokeaa agizo la hilo Mkuu wa Wilaya  ya Sikonge Mhe. Peres Magiri alisema kuwa tukio hilo linasikitisha sana na halikubaliki hata kidogo na kusisitiza kuwa pesa zote zitarudishwa kwa wahusika huku akiitaka Kuu ya Wilaya kuhakikisha wote walioshiriki wanachukuliwa hatua wakati huohuo alihaidi kutekeleza maagizo yaote kama yalivyotolewa  na mkuu wa Mkoa huku akitumia nafasi hiyo kuwatahadhalisha watumishi wengine kutojaribu mchezo huo na wananchi waliombwa kuwa na subra wakati utaratibu ukiwekwa vizuri.

Wakazi wa Sikonge wakijipanga kununua vitambulisho vya wajasiliamali.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Sikonge Bi. Martha Luleka alilaani vikali kitendo hicho kwa kusema kuwa ni tukio la aibu lisilokubalika kwani mbali na kuwakera wao kama viongozi pia limewakera wananchi. Hivyo basi kwa kufuata taratibu za kiutendaji mtuhumiwa huyo atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwemo kueleza alipopata maelekezo hayo na kubainisha wafuasi ambao amekuwa akishirikiana nao kufanya tendo la namana hiyo.

Akitolea ufafanuzi wa namna alivyokusanya pesa zaidi ya kiasi kilichobainishwa na Serikali, Mtendaji Bwana  Jerad alisema kuwa kiasi kilichotozwa kilikuwa ni shilingi elfu ishirini na gharama ya shilingi elfu moja ilitokwa ili kutolea nakala ya kitambulisho huku elfu 5 ilitozwa kama faini  kwa watu walioleta ubishi ikiwemo lugha ya kashfa hivyo kupelekea jumla ya gharama kufikia shilingi elfu ishirini na sita.

Mkuu wa mkoa alifanya ziara ya kuhamasisha wajasiliamali wadogo wadogo katika kata ya Kitunda na Kipili zilizoko Wilayani Sikonge Mkoani Tabora, ambapo alitoa semina kwa wananchi juu ya umuhimu wa kuwa na vitambulisho hivyo kwani ni njia pekee ya wananchi kuepukana na bugdha katika biashara zao. Sababu ikiwa ni kutambuliwa na serikali na kuwekewa utaratibu mzuri ikiwemo maeneo ya kufanyia biashara.

Wananchi wengi walipokea kwa muitikio mkubwa sanjari na kununua vitambulisho hivyo maalufu kama Viparata huku wasio kuwa na pesa wakijiorodhesha majina yao ili kuanza utaratibu wa kulipa kidogokidogo na watakapokamilisha waweze kupatiwa Vitambulisho vyao rasmi.

IMETOLEWA NA 

KITENGO CHA TEKINOLIJIA HABARI NA MAWASILIANO (TEHAMA)

          SIKONGE.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa