• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

Imewekwa: June 6th, 2025


 Na Edigar Nkilabo,


Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi imevijumuisha vijiji 16 kati ya 71 vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora katika uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi utakaowawezesha wananchi kushiriki kupanga matumizi ya ardhi yao ili waweze kuitumia ardhi hiyo kwa tija katika shughuli mbalimbali za uzalishaji na kuinua hali zao za maisha.

Hayo yamesemwa Wilayani Sikonge na Afisa Ardhi Mkuu kutoka Tume ya Taifa ya Mipango na Matumizi ya Ardhi(NLUPC), Nyirembe Munasa ambapo amesema zoezi hilo ni utekelezaji wa ilani ya CCM inayosisitiza kuwapa wananchi haki ya umiliki wa ardhi ambao utawawezesha kupata hati za kimila na kufanya shughuli zao za maendeleo kwa tija.

“Eneo kubwa la Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge ni misitu na hifadhi ni eneo dogo la ardhi ambalo wananchi wanatumia kwa makazi hivyo nyenzo pekee ni kuandaa mipango shirikishi ya matumizi bora ya ardhi ili wananchi wapate maeneo kwa ajili ya kilimo cha tumbaku,uwindaji, maeneo ya huduma za jamii na makazi.Pia wananchi watapata hati za kimila ambazo zitawawezesha kukopa na kupata mitaji ya kufungua biashara na kujikwamua kiuchumi”amesema.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe.Cornel Lucas Magembe amesema programu hiyo ni jawabu la changamoto za wakazi wa Sikonge ambao wamekuwa wakikabiliwa na migogoro ya ardhi kutoka na mwigingiliano wa shughuli za kibinadamu.

“Kesi nyingi tunazotatua za migogoro ya ardhi viongozi zinatokana na kukosekana kwa mipango ya matumizi bora ya ardhi hivyo unakuta eneo la makazi hapo hapo kuna nyumba za ibada, maeneo ya masoko hayaeleweki naamini programu hii imekuja muda muafaka kwani migogoro itapungua kwa kiasi kikubwa kwakweli tunamshukuru Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutukumbuka Sikonge kupitia mradi huu unaotekelezwa na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi”amesema.

Kwa upande wao baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Kabanga ambao ni miongoni mwa wanufaika wa programu hii wamesema elimu waliyopatiwa katika mpango ambao ni shirikishi imewafumbua macho hivyo migogoro ya kugombea mipaka baina ya kijiji na kijiji haitatokea tena na kila mwananchi atapata haki ya kumiliki kipande chake cha ardhi kwa mujibu wa sheria.

Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi inatarajia kutekeleza zoezi hilo katika Halmashauri 21 zilizopo kwenye mikoa 14 kupitia programu ya upangaji matumizi ya ardhi katika vijiji 333 vilivyoandaliwa na Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

    June 14, 2025
  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

    June 06, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa