• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA YAKAMILISHA MAFUNZO YA UONGOZI NA USIMAMIZI WA VYAMA VYA USHIRIKA KWA WAKULIMA WA TUMBAKU SIKONGE.

Imewekwa: November 10th, 2024

Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania kanda ya Magharibi imetangaza kumalizika kwa mafunzo ya siku saba kwa wajumbe wa bodi na wawakilishi wa vyama vya ushirika vya msingi wilaya ya Sikonge. Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya ushirika na wakulima, ili kufikia malengo ya uzalishaji bora wa zao la tumbaku.

Mafunzo hayo yamejumuisha nyanja mbalimbali muhimu za ushirika, zikiwemo masuala ya rushwa katika vyama vya ushirika, elimu ya uhamiaji kwa wanaushirika, maadili ya viongozi, na mikataba ya kazi kwa watendaji wa vyama vya ushirika. Wajumbe walipata pia fursa ya kula kiapo cha uadilifu cha viongozi wa vyama vya ushirika wilayani Sikonge, kilichoongozwa na mwanasheria kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

Mgeni rasmi katika kuhitimisha mafunzo hayo, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tabora, Ndg. Said Juma Nkumba, amewaonya viongozi wa vyama vya ushirika kuacha tabia ya "uungu mtu" ili waweze kuwatumikia wanachama kwa haki na ufanisi. Alisisitiza umuhimu wa viongozi hao kuwa waadilifu, kuwa na maadili ya uongozi, na kuwa viongozi wanaopatikana kirahisi kwa wanachama wao.

Aidha, Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Tabora, Bw. Venace Msafiri, amewasihi wajumbe wa vyama vya ushirika kujiunga na bima ya kilimo. Amesema kuwa bima hiyo itawawezesha kulinda mitaji yao na shughuli zao za kilimo, hasa wakati wa majanga kama uhaba wa mvua au dhoruba, ambapo fidia inaweza kutolewa kwa uharibifu wa mazao yao.

Akifunga mafunzo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Mhe. Cornel Lucas Magembe, amesisitiza umuhimu wa kuanzishwa kwa SACCOs za wakulima wa tumbaku. Amesema kuwa SACCOs hizi zitasaidia wakulima kutatua changamoto zao za kifedha, huku wakiepuka vishawishi vya kuuza tumbaku  soko huria, jambo ambalo ni kinyume cha sheria. Mkuu huyo ameongeza kuwa SACCOs pia zitakuwa na manufaa kwa wakulima katika kujiandaa na msimu wa kilimo.

Mhe. Magembe ametumia jukwaa hilo kutoa hamasa kwa wakulima kuwa mstari wa mbele kuhamasisha wananchi wenzao kuhusu umuhimu wa kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024.

Wilaya ya Sikonge imekuwa ya kwanza kunufaika na mafunzo haya, ambapo zaidi ya wanachama 400 wa vyama vya ushirika kutoka mkoa wa Tabora wamepata elimu na ujuzi wa kuboresha shughuli zao za kilimo na ushirika.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA SIKONGE YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOPENDEKEZWA KUPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 13, 2025
  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa