• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

“SULUHU AMCOS” YAIBUKA KIDEDEA: MKUTANO MKUU WA WAKULIMA WA TUMBAKU SIKONGE.

Imewekwa: August 31st, 2024

Mkutano mkuu wa wakulima wa tumbaku wa chama cha msingi SULUHU uliofanyika leo, Agosti 31, 2024, wilayani Sikonge, katika kijiji cha Chang'ombe kata ya Mkolye kimepata umaarufu na kupongezwa kwa mafanikio yake makubwa mwaka huu. Mkutano huu, uliojaa hisia za furaha na matumaini, uliwashirikisha wakulima, viongozi wa AMCOS, na Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Tabora Ndg. Venance Msafiri,ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo wa mwaka.

Katika mkutano huo, chama cha SULUHU kimepata wasaa wa kusoma mapato na matumizi ya fedha zake, huku wakionesha uwazi wa hali ya juu katika usimamizi wa rasilimali. Hali hii ilipokelewa vizuri na wajumbe wa mkutano, ambao walithibitisha utendaji mzuri wa chama hicho katika kuendesha shughuli zake. Mrajisi Msaidizi alitoa ahadi muhimu kwa chama hicho, akisema kuwa atahakikisha usajili wa kudumu unapatikana mapema, jambo ambalo litazidi kuimarisha na kuthibitisha uwepo wa chama hicho katika mfumo wa kilimo cha tumbaku.

Katika tathmini ya mwaka huu, imebainika kuwa chama cha SULUHU kimefanikiwa kulipa wakulima kwa asilimia 92.5 ya malipo yao.Ikiwa ni kiwango kikubwa cha kuridhisha, ikilinganishwa na viwango vya kawaida vya kulipa. Mafanikio haya yameongeza matumaini kwa wakulima na kuimarisha imani yao katika usimamizi wa chama chao.

Hata hivyo, Mrajisi Msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Tabora Ndg. Venance Msafiri hakukosa kutoa kauli kali kuhusu suala la utoroshaji wa tumbaku.Amekemea tabia hii ambayo imekuwa ikikumba sekta ya kilimo cha  tumbaku nchini, akisema kuwa ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya chama na ustawi wa wakulima. Amewaaasa viongozi wa AMCOS na wakulima kuhakikisha kwamba tabia hiyo inakomeshwa ili kuweza kupata faida kamili kutokana na  kilimo cha tumbaku na kufikia malengo ya maendeleo ya kilimo katika eneo hilo.

Katika hatua nyingine amewapongeza kwa dhati viongozi wa Amcos kwa kutekeleza kwa haraka wazo la uanzishwaji wa Saccos ikiwa ni hatua muhimu sana katika kupambana na hali duni ya uchumi wa wakulima wa tumbaku kwa kutoa mikopo yenye riba nafuu itakayoimarisha uchumi wa wakulima hao.

Kwa ujumla, mkutano huu umekuwa na mafanikio makubwa kwa chama cha SULUHU, ukiashiria mwanzo mpya wa matumaini na maendeleo katika kilimo cha tumbaku wilayani Sikonge. Wakulima wameonesha kuridhika na usimamizi bora wa chama chao, huku viongozi wakiahidi kuendelea kuboresha huduma na kupambana na changamoto zilizopo.

USHIRIKA! PAMOJA TUJENGE UCHUMI.

“Serikali za Mitaa,Sauti ya Wananchi,Jitokeze kushiriki Uchaguzi.”


Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WALIMU ZAIDI YA 200 WA SHULE ZA MSINGI WILAYANI SIKONGE WAPEWA MAFUNZO YA KUFUNDISHA SOMO LA KIINGEREZA.

    May 21, 2025
  • CCM, MKOA WA TABORA YAWAHIMIZA WAZAZI NA WALEZI WILAYANI SIKONGE KUCHANGIA CHAKULA SHULENI

    May 19, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA SIKONGE YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOPENDEKEZWA KUPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 13, 2025
  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa