• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

SIKONGE YAFUNIKA UZINDUZI WA SEMA USIKIKE

Imewekwa: March 12th, 2018

SIKONGE YAFUNIKA UZINDUZI WA SEMA USIKIKE

Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge imezindua rasmi Kampeni ya SEMA USIKIKE dhidi ya Rushwa, Mimba na Ndoa za Utotoni katika Viwanja vya TASAF. Uzinduzi huo ambao ni wa Kimkoa umefanyika leo kwa kuwashirikisha wanafunzi wenyewe ambao wamefikisha jumbe mbalimbali kuhusu Rushwa na Mimba za utotoni kupitia Maigizo, Nyimbo, Ngonjera, Ngoma za jadi na Mashahiri.

Mkurugenzi wa Taasisi ya “Creative Plan” yenye kali mbiu ya SEMA USIKIKE, ndugu Juma Mtetwa akasema, “hakika Sikonge mmefunika, katika sehemu zote tulizopita sijaona kama Sikonge.”  Aliyasema hayo baada ya kuona jumbe mbalimbali zilizowasilishwa na wanafunzi wenyewe, na akasema hili ndilo lengo kuu la kauli mbiu yao.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Simon Ngatunga alifurahishwa sana na maandalizi waliyoyaonesha wanafunzi katika uzinduzi huo. “Mataifa makubwa duniani yaliyopiga hatua mbalimbali za kimaendeleo, (mfano. Japan) yalianzia katika msingi wa watoto, hivyo mtoto anakua akijua jambo Fulani ni baya kwa Nchi yangu (mfano. Kutolipa kodi ya Nchi)”, alisema Mkurugenzi huyo.

…"Hivyo kwa kuwashirikisha watoto wenyewe katika masuala ya Rushwa, Mimba na Ndoa za utotoni ni kuwajengia msingi imara utakaowafanya watoto hao kuwa imara siku za badae watakapokuwa viongozi.”  Aliyasema haya na kisha kumkaribisha Mgeni Rasmi ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Mhe. Peres Magiri.

 Mgeni Rasmi aliwapongeza sana walioandaa zoezi zima la uzinduzi na walioshiriki hasa Mkurugenzi wa “Creative Plan”. Pia aliwaeleza wananchi pamoja na watumishi kuwa Mgeni Rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Mhe. Agrey Mwanri lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake hakuweza kufika hivyo alimuomba amuwakilishe katika hafla hiyo.

Aidha, Mgeni rasmi alisema, “Rushwa ni adui wa haki, hata ninyi mmeyaeleza katika maigizo yenu hapa, hata Rais wa Nchi analikemea na kupambana juu ya hili kila siku na nyote ni mashahidi, hebu tumpigie makofi Mhe. John  Magufuli.” Alisisitiza kushirikiana kwa pamoja juu ya kupambana na rushwa kwani TAKUKURU peke yao hawatoweza.

Akizungumzia jambo la Mimba za utotoni alisema, “wanafunzi ngojeni niwafundishe mbinu nyingine ya kuepukana na vishawishi vya mafataki, akikusemesha mjibu kwa lugha ya kizungu kwani waliowengi hawajui lugha hiyo, mwisho wa siku ataishia kusema… anajifanya msomi…, acheni waseme hivyo lakini umeshamuepuka.” Aliendelea kusisitiza kuwa kwa kuwaepuka hao mafataki na watu wa aina hiyo, tutapata Wabunge, Mawaziri na hata Marais.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA TEHAMA

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa