• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

SIKONGE MJINI YAPAA KUTOKA ASILIMIA 5 HADI 62

Imewekwa: March 22nd, 2018

Na Halidi Nyange na Mwatebela Gadi


Mji wa Sikonge ni miongoni mwa miji iliyopo katika maeneo yenye hali ya Kitropiki, hivyo upatikanaji wa maji ya ardhini ni mgumu. Hata hivyo, kulingana na jitihada za Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge imeendelea na kupambana na uhaba wa maji katika mji huo.

Halmashauri hiyo imeweza kuboresha upatikanaji wa maji kutoka asilimia 5 za upatikanaji wa maji Mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 62 za upatikanaji wa maji Mwaka 2017 katika mji wa Sikonge. Hatua hiyo imefikiwa kwa kujenga Magati na kusambaza mabomba ya maji majumbani kutoka katika chanzo cha maji ya bwawa la Utyatya lililopo umbali wa kilomita 12.6.

Aidha, Mhandisi wa Maji Wilaya, Paschal Ngunda alisema, “hadi kufikia 2025 tunategemea kufikia asilimia 100 za upatikanaji wa maji katika mji wa Sikonge.” Mhandisi huyo alisisitiza utunzaji wa vyanzo vya maji hasa mabwawa ili viweze kudumu na kuwahudumia wananchi.

Hayo yalisemwa katika kuhitimisha Wiki ya Maji katika Kijiji cha Utyatya Kata ya Kisanga ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Peres Magiri. Wiki hiyo ya maji Duniani yenye Kauli mbiu, Hifadhi Maji na Mfumo wa Ikolojia kwa Manufaa ya Jamii ilianza tarehe 16 Machi na kuhitimishwa 22 Machi 2018.

Katika kuhitimisha wiki ya maji, Mgeni rasmi alikagua upandaji wa miti kandokando ya bwawa la maji Utyatya pamoja na kushiriki upandaji wa miti katika kijiji hicho. Akifunga wiki ya maji Duniani alisema, “shughuli za ujenzi wa makazi na kilimo katika maeneo ya bwawa lolote lililopo Wilaya ya Sikonge, ziondolewe mara moja, wavamizi wakamatwe mara moja na nyumba zivunjwe! sihitaji kutoa siku.”

Aidha, katika kilele cha wiki hiyo mgeni rasmi alizindua Gati moja la Maji Mjini Sikonge na kuwasisitiza wananchi juu ya utunzaji wa miundombinu ya maji ili upatikanaji wa maji uwe endelevu. Ujenzi wa Gati hilo umegharimu Milioni nne. Wananchi hasa kina mama wamefurahia sana uzinduzi wa gati hilo kwani litarahisisha upatikanaji wa maji na kwa gharama ndogo ya shilingi 50 kwa lita 20, kwani awali walikuwa wakinunua maji kwa shilingi 500 kwa lita 20.



IMEANDALIWA NA KITENGO CHA TEHAMA

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa