• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

SHULE BINAFSI KILIO CHA WENGI-SIKONGE

Imewekwa: May 15th, 2019

ESFR.pdf

SHULE BINAFSI KILIO CHA WENGI-SIKONGE.

 

Wawezeshaji kutoka ESRF waliokaa kulia wakijadiliana na wajumbe kwenye semina ya fursa za uwekezaji  iliyofanyika Ofisi ya Mkurugenzi - Sikonge.

Timu ya wawezeshaji kutoka Shirika la Economic and Social Research (ESRF) yatua Sikonge kujadili fursa za uwekezaji.

Timu hiyo iliyoundwaa na wajumbe watatu akiwemo Dr. Bohela Lunogelo, Ben Mtalemwa na Prof. godwin Mjema,  ilifanikiwa kukutana na wawakilishi wa wafanyabiashara, wakuu wa Idara pamoja na vitengo  vilivyopo Wilayani hapa na kufanya semina iliyolenga kubainisha  fursa zinazoweza kutumiwa na wadau wanaohitaji kuwekeza Wilayani Sikonge.

Miongoni mwa fursa iliyopewa kipaumbele na wajumbe waliohuzulia semina hiyo ilikuwa ni uanzishwaji wa shule binafsi za msingi zinazotumia mtaala uliokwenye lugha ya kiingereza ambapo wajumbe 10 walichangia kuwa ni miongoni mwa jambo linalopewa kipaumbele kikubwa. Wilaya ya Sikonge haina shule ya namna hiyo hata moja jambo linalowalazimu wazazi kuwapeleka watoto wao nje ya Wilaya hii na hata mikoa mingine ikiwemo Shinyanga- Kahama.

Hali hii imekuwa ni kilio cha muda mrefu kwa wakazi wa Sikonge ambao wamekuwa na uhitaji mkubwa wa huduma hiyo, hivyo kuwakaribisha wadau wote wenye uwezo wa kuwekeza katika shule binafsi kuchangamkia fursa hiyo.

Akielezea kivutio kinachopatikana katika uwekezaji huo Martin Ukongo ambaye ni Afisa Ardhi alisema kuwa gharama za upatikanaji wa eneo zipo chini kulinganisha na sehemu zingine na tayari Halmashauri imetenga eneo kubwa kwa ajili ya uwekezaji huo ambapo ili kuwavutia wawekezaji mita moja za mraba huuzwa kwa thamani ya shilingi elfu moja tu.

Mbali na fursa hiyo pia kulijadiliwa fursa mbalimbali zinazopatikana Wilayani hapa ambazo miongoni mwao zilikuwa ni kujenga kiwanda kwa ajili ya mazao ya Nyuki, kilimo cha Umwagiliaji, kiwanda cha Mafuta, Hoteli na huduma za kitalii na uanzishaji wa Mashamba makubwa ya Tumbaku, Alizeti na Karanga, ambapo zinaweza kutumiwa na wawekezaji kwani maeneo yapo ya kutosha.

Majadiliano yakiendelea- Semina ya Fursa za Uwekezaji Sikonge.

Akitoa maelezo namna Sikonge inavyoweza kuzitangaza Fursa zilizopo, muwezeshaji Dr. Bohela Lunogelo alisema kuwa mawazo yote yaliyotolewa na wadaau yatawekwa kwa pamoja na machapisho mbalimbali yatatolewa ili yaweze kuwafikia wadau wa uwekezaji, pia alishauri kutumia machapisho na makala ambazo zitarushwa kwenye mtandao wa kijamii lengo likiwa ni kufikisha ujumbe sehemu mbalimbali kama njia ya kuwakaribisha wawekezaji.

Naye injinia Paschal Ngunda aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi alitoa shukurani kwa wawezeshaji kutoka ESRF kwa kusema, “mambo mengi hayafanikiwi kwa kuwa hayana miongozo sahihi” hivyo alishukuru timu hiyo kwa kuwapa miongozo sahihi itakayofungua fursa za uwekezaji Wilayani Sikonge.

IMEANDALIWA NA 

          KITENGO CHA TEKNOLOJIA HABARI NA MAWASILIANO (TEHAMA)

          SIKONGE.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa