• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

SHIRIKA LA MDH LAENDESHA MAFUNZO YA ELIMU YA AFYA KWA WAHESHIMIWA MADIWANI, WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI WILAYANI SIKONGE.

Imewekwa: May 2nd, 2024

Shirika lisilokuwa la kiserikali linalojihusisha na uboreshaji wa huduma ya afya kwa umma(MDH) limeendesha mafunzo kwa waheshimiwa madiwani,watendaji wa kata pamoja na watendaji wa  vijiji juu ya elimu ya afya katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Sikonge.

Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo Bw.Simon Malley,Afisa takwimu toka MDH amesema upo umuhimu kwa viongozi katika kata na vijiji kutilia mkazo suala zima la afya ya akinamama wajawazito  kutokana na changamoto za kuanza kliniki ya ujauzito  kwa wakati pamoja na kufanya kipimo cha marudio .Amesisitiza ni muhimu kuhamasisha na kuelimisha kuhusu jambo hilo ili kuwalinda wanawake na changamoto za uzazi.

Kwa upande wake Bi. Veronica Ferdinand,Afisa lishe wilaya ya Sikonge amesisitiza umuhimu wa lishe bora kwa mtoto  ili kuepukana na athari za udumavu  ambazo huathiri sana watoto katika makuzi na utendaji wao darasani,hivyo amesisitiza umuhimu wa wazazi kuzingatia mlo wa mtoto. “Mtoto anayekua anahitaji kula si chini ya mara tano kwa siku na sio kula tu bali kula chakula chenye virutubisho muhimu kwa ajili ya ukuaji wake.” Amesema Bi. Veronica.

Akiwasilisha mpango  mkakati kwa ajili ya kuimarisha huduma za  afya ya mama na mtoto,Mratibu wa Afya ya uzazi na mtoto Bi. Lenatha Mondo amesema moja ya njia ya kuimarisha afya ya mama na mtoto ni pamoja na kuboresha elimu ya afya ya uzazi  katika vituo vya kutolea huduma za afya,huduma za mkoba zifanyike katika maeneo yasiyoweza kufikika kirahisi pamoja na maeneo ambayo hayana  vituo  vya kutolea huduma za afya na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika maduka ya  dawa  na kukomesha huduma za upimaji na kuzalisha zinazofanywa kinyume na utaratibu katika maduka  haya.

Aidha mada zingine zilizowasilishwa ni pamoja na elimu juu ya maambukizi ya virusi  vya Ukimwi na Ukimwi.Bado ipo haja ya kuiunga mkono Serikali katika mapambano inayoyaongoza dhidi ya ugonjwa huu wa hatari hasa kwa kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto pamoja na kuzuia maambukizi mapya katika jamii kwa ujumla.

Akifunga mafunzo hayo Mhe. Rashid Magope,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge ametoa wito kwa shirika la MDH kupanua wigo ili kuwafikia viongozi wengi zaidi hasa waheshimiwa madiwani kwani uwakilishi wao na ushawishi wao katika maeneo yao utasaidia sana katika kuleta mwamko  juu ya afya ya mama na mtoto kwa haraka.



Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA MTEULE WA WILAYA YA SIKONGE MHE.THOMAS MYINGA ALA KIAPO KUANZA KAZI RASMI AKIRITHI MIKOBA YA MTANGULIZI WAKE MHE.CORNEL MAGEMBE

    July 02, 2025
  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

    June 14, 2025
  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa