• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

SERIKALI YAWAJALI WALIMU

Imewekwa: May 9th, 2019

SERIKALI YAWAJALI WALIMU

Kata ya Usunga iliyopo Wilayani Sikonge ni miongoni mwa kata zilizofaidika na miradi ya TEA ambapo katika shule ya Sekondari Usunga wamejengewa nyumba bora ya waalimu ijulikanayo kama six  in one.

Hivi karibuni kamati ya Fedha ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge ikiongozwa na Mhe. Peter Nzalalila ambaye ni mwenyekiti wa Halmashauri walitembelea shuleni hapo na kukagua ujenzi huo ambao tayari umekamilika na hatua za kwanza za kukabidhi kwa Muhandisi wa Wilaya zilikuwa zimekamilika.

Wakiwa katika ukaguzi wa Nyumba hiyo wajumbe wa kamati ya fedha walitoa pongezi mbalimbali kwa serikali ya awamu ya tano ilivyojitolea kuwajali watumishi wake kwani kwa kufanya hivyo itaongeza ufanisi katika utendaji kazi wa watumishi.

Mhe. Nzalalila alitoa maagizo kwa mwalimu mkuu wa shule ya sekondari usunga kuhakikisha inafanya utaratibu wa kuwapata walimu sahihi ambao watapewa nyumba hizo ili waanze kuzitumia. Akiongeza “kusiwe na upendeleo kwenye ugawaji wa nyumba hizo wapewe wanaostahili”.

Akichangia swala hilo Mhe. Zena Aruna ambaye ni diwani viti maalumu CCM alisema kuwa serikali imetoa pesa nyingi katika mradi huo hivyo mtumishi yeyote atakayekabidhiwa nyumba hiyo ni jukumu lake kuhakikisha anaitunza vizuri na kwa kuzingatia usafi, “hatutavumilia kuona mazingira ya nyumba hii yanaharibiwa, mtumishi yeyote atayepewa nyumba hii ahakikishe anaitunza kama anavyotunza nyumba yake”.

Akitoa pongezi zake kwa serikali Mwenyekiti wa ujenzi wa nyumba hiyo alisema kuwa mradi huo umenufaisha wazawa kwani ulikuwa ni chanzo kizuri cha ajira kwa wakazi wa eneo hilo.

 Sanjari na hayo mradi huu pia utasaidia katika kuinua kiwango cha ufauru shuleni hapo kwani utawaweka walimu karibu na mazingira yao ya kazi jambo litakalosaidia kuwa karibu na wanafunzi na kugundua kwa haraka mabadiliko yeyote yatakayojitokeza.

baadhi ya wajumbe wa kamati ya Fedha wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe kamati ya ujenzi nyumba ya walimu kata ya Usunga.

“Hatutakubali mwalimu amepewa nnyumba nzuri namna hii alafu atoe wanafunzi wenye ziro” alisema Mhe. Juma Mdulla akitoa onyo kwa walimu wa shule ya sekondari Usunga.

Kamati hiyo ilitoa pongezi nyingi kwa raisi wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kuwa karibu na wananchi wake na kuwajali watumishi, pia kwa mbunge wa jimbo la Sikonge Mhe. Joseph Kakunda kwa kutimiza ahadi zake na pia waliwaasa wananchi kuwa wanajitolea katika miradi inayokuja kwasababu inawagusa wao moja kwa moja.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

    June 14, 2025
  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

    June 06, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa