• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

SEKTA BINAFSI ZINAZOSAMBAZA NISHATI YA UMEME VIJIJINI ZAAGIZWA KUZINGATIA BEI ELEKEZI

Imewekwa: July 19th, 2019

SEKTA BINAFSI ZINAZOSAMBAZA NISHATI YA UMEME VIJIJINI ZAAGIZWA KUZINGATIA BEI ELEKEZI.

Sekta binafsi zilizopewa kibali cha kuzalisha nishati ya umeme zaagizwa kufuata bei elekezi iliyotolewa na Serikali wakati wa kuuza vifaa vya umeme pamoja na usambazaji wa Umeme kwa wananchi.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu alipofanya ziara Wilayani Sikonge ili kukagua namna ambavyo mradi wa Umeme Vijijini (REA) unavyowasaidia wakazi wa vijijini, na kufanikiwa kutembelea vijiji vya Kikungu kata Chabutwa, Kata ya Ipole na Kijiji cha Lukula kilichopo kata ya kitunda ambacho kinapata umeme wa Jua.

Akitoa bei elekezi Mhe. Mgalu Alisema kuwa mwananchi atachangia shilingi elfu ishirini na saba (27,000/=) tu ili kupata nishati ya umeme lakini gharama za kusambaza nyaya katika nyumba (wirering) zitakuwa juu ya mteja mwenyewe na baada ya hapo atavutiwa umeme na sio vinginevyo.

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu (Mwenye Mtandio Mwekundu) alikata utepe kuashiria uzinduzi wa nishati ya umeme kuanza kutumika katika msikiti uliopo kijiji cha Kikungu Kata ya Chabutwa Wilayani Sikonge.

Akiwa kata ya Kitunda pia alifanikiwa kukagua mradi wa PowerCorner ulio chini ya sekta binafsi ambao unazalisha umeme kwa kutumia nishati ya jua, na kumtaka muwekezaji huyo kutoa huduma kwa kuzingatia bei elekezi iliyowekwa na serikali kwasababu serikali iliingia ubia na kampuni hiyo kwa kutenga kiasi cha shilingi Bilioni 3 ili kufaniisha mradi huu. Vilevile alipita kukagua namna ambavyo mradi huo umekuwa fursa kwa wananchi kujikwamua kiuchumi ambapo alizungumza na mafundi wa kuchomelea chuma wanaotumia nishati hiyo.

Sanjari na hayo pia Mhe. Mgalu aligawa Swichi ya Umeme aina ya uwamita kwa watu wenye ulemavu ikiwa ni mpango wa serikali kuwasaidia wenye ulemavu, wajane na wazee wenye umri mkubwa ili nao waweze kupata nishati ya umeme. Huku akiitaka EWURA kujenga utaratibu wa kuwatembelea wananchi wa vijijini mara kwa mara ili kubaini changamoto na kuzitatua mapema.

Katika ziara hiyo pia aliambatatana na wenyeji wake akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Peter Nzalalila, Mkurugenzi Bi. Martha Luleka, Katibu Tawala Wilaya Renatus Mahimbali pamoja na mbunge wa jimbo la SIKONGE Mhe. Joseph Kakunda ambaye alitoa shukrani zake kwa serikali kwa kuwatoa wananchi gizani kwani wamekuwa wakisubiri kupatiwa nishati ya umeme kwa muda mrefu na sasa umeme unawaka hadi majumbani.

Vilevile aliongeza kuwa wananchi waitumie fursa hiyo vizuri ili kujiendeleza na shughuli za kiuchumi, kwani utawasaidia kurahisisha kazi zao sambamba na kuongeza muda wa kufanya kazi.

Miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa ilikuwa ni kijiji cha kikungu ambapo alizindua umeme katika ofisi ya Mtendaji wa Kata, Nyumba ya Mzee Issa pamoja na Nyumba ya Ibada (Msikiti) pamoja na kukabidhi Swichi kwa Mtu mwenye ulemavu.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa