• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

RC MWANRI ATAKA USIMAMIZI MAKINI MIRADI YA MAENDELEO SIKONGE

Imewekwa: May 22nd, 2019

RC MWANRI ATAKA USIMAMIZI MAKINI MIRADI YA MAENDELEO SIKONGE

Na Eveline Odemba, Sikonge

MKUU wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ameagiza Wataalamu wa halmashauri ya wilaya ya Sikonge kufuatilia utekelezakaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani humo kwa umakini mkubwa ili kuepusha udanganyifu.

Alitoa agizo hilo juzi alipofanya ziara maalumu ya ukaguzi wa  miradi ya shule inayotekelezwa katika na serikali katika halmashauri hiyo.

Akiwa katika shule ya Msingi Ulilwansimba alikagua ramani za majengo na kugundua kuwa ramani haikufuatwa hasa katika jengo la vyumba viwili vya madarasa ambapo ramani yake ilionesha kuna chumba cha ofisi ya walimu lakini kwa namna lilivyojengwa hakuna ofisi hiyo.

Alibainisha kuwa kukosekana kwa ufuatiliaji makini wa miradi inayotekelezwa na Serikali katika halmashauri ndiyo chanzo cha uharibifu wa miradi, hivyo akaagiza Ofisa Elimu wa shule za msingi na Kaimu Mhandisi wa wilaya hiyo kufuatilia kila hatua ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Aliagiza Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Martha Luleka kuwasiliana na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili kuomba kupatiwa Mhandisi mwingine wa ujenzi ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa miradi hiyo baada ya aliyekuwepo kuhamishiwa Wakala wa Barabara za Mjini na Vijiji (TARURA).

Mhe. Agrey Mwanri Mkuu wa Mkoa wa Tabora aliyevaa shati rangi ya Bahari akitoa maelekezo alipotembelea miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa Wilayani Sikonge.

‘Sikonge mnafanya vizuri katika kutekeleza miradi ya maendeleo tatizo lililopo ni kukosekana  kwa umakini katika ufuatiliaji, ndiyo maana wakandarasi wanafanya wanavyotaka, wataalamu kuweni makini sana’, alisema.

Aidha Mkuu wa Mkoa alitembelea shule ya Sekondari ya Kamagi ambapo alisisitiza suala la kubana matumizi katika utekelezaji miradi hiyo sambamba na kuangalia ubora wa vifaa vinavyotumika.

Ili kufanikisha miradi hiyo alipendekeza kufuatwa kwa ramani iliyopo ikiwemo kuhakikisha matofali yanamwagiliwa asubuhi na jioni ili kupata ubora unaohitajika huku akiwataka kutokata miti ovyo kuhakikisha mfumo wa maji na umeme unawekwa kabla ya jengo kupigwa plasta.

Aidha alimwagiza Ofisa Elimu Sekondari Yusuph Hamza kuhakikisha mbao zisizo na ubora  zinarudishwa kwa muuzaji kwani hazifai kutumika.

Akijibu hoja hiyo Kaimu Mhandisi wa Wilaya Bi. Joyce Faustine alisema kuwa walichukua maamuzi ya kuamishia ofisi kwenye jengo la pili kutokana na kuwa jengo la kwanza kupakana na jengo la zamani ambalo ofisi tayari ilikuwepo.

Naye Mkuu wa Wilaya hiyo Peres Magiri alishukuru kwa niaba ya Wilaya na kuahidi kutekeleza yale yote yaliyoagizwa na Mkuu wa mkoa huku akibainisha kuwa ataweka kambi katika Shule ya Kamagi ili kuhakikisha fedha zilizotolewa na serikali zinatumika vizuri na mradi unakamilika kwa wakati.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa