• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

RC. BALOZI DKT. BURIAN ATEMBELEA WILAYA YA SIKONGE KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WAKULIMA WA TUMBAKU KATA YA KISANGA.

Imewekwa: November 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian amezuru Wilayani Sikonge akiongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kusikiliza na kutatua kero za Wakulima wa Tumbaku hususani katika Kata ya Kisanga.

Akifungua kikao hicho Mhe. Balozi Burian amesema kilichosababisha kuja Sikonge ni baada ya kujitokeza kwa sintofahamu katika Chama cha Amcos Kisanga hasa baada ya kuuza tumbaku yao na wakulima kushindwa kupokea  malipo ya jasho lao kwa sababu ya deni linalowakabili katika benki ya NMB Sikonge.

Mhe.Burian amesikitishwa sana na mwenendo wa kilimo cha tumbaku Sikonge hasa baada ya kuona jinsi wakulima walivyojituma kwa juhudi na kuishia kulipa madeni tu.

Akiongoza kikao hicho kilichohudhuriwa na wakulima pamoja na viongozi wao amesema haki ya wale waliolima lazima ipatikane “Hatuwezi kuwavumilia watu wanao wadhulumu wakulima” amesema Balozi Batilda.

Kwa upande wao wakulima wakiwasilisha malalamiko yao  mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Tabora wamesema Chama cha Msingi Amcos Kisanga hakijawalipa wakulima haki yao na hii inasababishwa na kuwa na deni kubwa benki wanakochukua ruzuku,lakini pia kuna wakulima wasio waaminifu wanaochukua ruzuku lakini baada ya kuvuna tumbaku hukimbilia  kuuza tumbaku soko huria hivyo kusabisha deni kubwa la fidia ya ruzuku kwa wakulima waaminifu.

Aidha imebainika kuwa viongozi wa chama cha msingi Amcos Kisanga kutumia madaraka yao vibaya kwa kushiriki kuuza tumbaku nje ya chama cha msingi lakini pia kushidwa kuwasomea deni wanalodaiwa wakulima katika chama cha Amcos Kisanga.

Baada ya kuwasikiliza wakulima na changamoto zao Mhe. Mkuu wa Mkoa aliahirisha kikao na kuamuru mara moja kuketi kama kamati ya uchunguzi ya mkoa ili kuleta suluhu ya kero zinazowakabili wakulima hao.

Baada ya kamati ya uchunguzi kuketi Zaidi ya masaa Matano ikiongozwa na Mhe. Dkt. Burian imebaini mambo Matano,Utoroshaji mkubwa wa tumbaku ili kukwepa  kulipa deni la chama cha msingi,Changamoto katika chama cha Kisanga Amcos,imebaninika kumekuwa na utakatishaji mkubwa wa fedha,Ukopeshaji wa pembejeo wenye upendeleo,Utoaji mikopo wenye upendeleo,utoaji wa pembejeo usiozingatia uwezo wa mkulima,Udhaifu katika usimamizi wa tumbaku toka kwa Afisa ushirika na matumizi mabaya ya madaraka hasa katika kufanya maamuzi mbalimbali.

Akifunga kikao hicho Dkt. Burian ameamuru watumishi watano wanaohusika na masuala ya chama cha msingi Amcos na ushirika kuwekwa chini ya ulinzi ili kusaidia uchunguzi wa kero zilizobainika.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa