• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

PIKIPIKI 10 ZENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 35 ZAKABIDHIWA KWA WATENDAJI WA VIJIJI

Imewekwa: September 3rd, 2025


Na Edigar Nkilabo – SikongeDC


Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge imewapatia Watendaji 10  wa Vijiji pikipiki za mkopo usiokuwa na riba kwa lengo la kuwawezesha kufika kwa wakati katika Vitongoji vyao na kutoa huduma bora kwa wanachi wa maeneo yao.

Akizungumza wakati wa zoezi la kukabidhi pikipiki hizo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Ndugu Selemani Pandawe amesema programu hii inalenga kutatua changamoto  ya usafiri kwa Watendaji wa Vijiji.

“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya tumeanza na hizi pikipiki 10 kwa kuwapatia Watendaji wa Vijiji wenye maeneo makubwa na yambali lengo ni kuwawezesha kufanya kazi ya serikali kwa wepesi na baadae watakapomaliza mkopo na kutunza chombo hiki vizuri tutahamisha umiliki kutoka Halmashauri na kuwa pikipiki zao”amesema Mkurugenzi Mtendaji.

Naye Mkuu wa Divisheni ya Utawala na Rasilimali Watu Ndugu Nico Kayange amesema Mpango huu wa ununuzi wa Pikipiki za mkopo usiokuwa na riba  ulianza na Watendaji wa Kata na baada ya kukamilisha marejesho , Halmashauri imeagiza pikipiki zingine 10 kwaajili ya Watendaji wa Vijiji.

“Tulianza kutatua changamoto ya usafiri kwa Watendaji wetu wa Kata na sasa tumeanza kuwakopesha Watendaji wa Vijiji ili na wao waweze kuyafikia maeneo yao ya kiutendaji kwa wakati na kutoa huduma”

“Pikipiki zote 10  tulizonunua zimegharimu zaidi ya shilingi milioni 35 na chimbuko la fedha hii ni fedha iliyobaki baada ya kununua gari ya Mkurugenzi Mtendaji ndipo menejimenti ilipoamua kununua pikipiki na kuwakopesha Watendaji wetu , tukianza na wale wa Kata na sasa tunawapatia hawa wa Vijiji ambao wataulipa mkopo huu kwa kipindi cha miaka 2 kisha kukabidhiwa moja kwa moja pikipiki hizo”amesema.

Kwa uapnde wake Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe.Thomas Myinga ameipongeza Halmashauri kwa ubunifu huo wa kutatua changamoto za usafiri kwa Watendaji wake wa Kata na Vijiji kwani fedha hiyo ingeweza kupangiwa matumizi mengine.

“Binafsi niwapongeze kwa kuamua kuwasaidia usafiri Watendaji wetu maana Jiografia ya Wilaya yetu ni kubwa utendaji wake bila usafiri ni mgumu, fedha hizo baada ya kubaki kwenye ununuzi wa gari ya Mkurugenzi Mtendaji mngeweza kufanyia shughuli nyingine lakini kwakuwajali Watendaji wetu mkaona mtatue changamoto ya usafiri ili wakatoe huduma bora kwa wananchi wetu”amesema Mhe.Myinga.

Aidha Mhe.Myinga amewataka Watendaji wa Vijiji kuzitunza pikipiki hizo na kuzitumia kwa manufaa ya umma na binafsi kwakuwa mkataba uko wazi baada ya marejesho watapewa umiliki wa pikipiki hizo.\

“Mtunze hivyo vyombo vya moto kama mali yenu ili baada ya kukamilisha malipo muwe na kumbukumbu lakini pia muendeshe kistaarabu haina haja ya kukimbia sana , ukikimbia sana ukianguka na pikipiki utapoteza maisha au kuwa mlemavu”amesisitiza.

Akishukuru kwa niaba ya Watendaji wa Vijiji waliopata pikpiki hizo Ndugu Enock Mangu Mtendaji wa Kijiji cha Idekamiso amesema wanaishukuru sana Halmashauri kwa kuwapatia pikipiki hizo kwani zitawarahisishia kazi kwa kufika katika Vitongoji vyao na kutoa huduma kwa wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • PIKIPIKI 10 ZENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 35 ZAKABIDHIWA KWA WATENDAJI WA VIJIJI

    September 03, 2025
  • NG’OMBE ELFU HAMSINI WACHANJWA CHANJO YA HOMA YA MAPAFU KWA BEI YA RUZUKU YA SH.500 HUKU KUKU ZAIDI YA LAKI NNE WAKICHANJWA BURE CHANJO YA KIDERI,NDUI NA MAFUA YA KUKU.

    August 29, 2025
  • USALAMA WA RAIA NA MALI ZAKE NI JUKUMU LETU SOTE WANANYAHUA

    August 26, 2025
  • WANAFUNZI 54 WAHITIMU MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA ( MGAMBO) WILAYANI SIKONGE

    August 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa