• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

“NATOA WITO KWA WATU WOTE HASA WANAUME KUJITOKEZA KUPIMA NA KUJUA HALI ZETU NA KUANZA KUTUMIA DAWA MAPEMA” MHE. CHACHA.

Imewekwa: December 1st, 2023

Na. Robert Magaka ,Sikonge – Tabora.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Simon Chacha alipokuwa akihutubia wananchi waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge.

Aidha Mhe. Chacha amewasihi wananchi kuitikia wito wa kauli mbiu ya Siku ya Ukimwi duniani unaosema “Jamii iongoze kutokomeza Ukimwi” kwa kujitokeza kwa hiyari kupima virusi vya Ukimwi na kuanza kutumia dawa mapema kwa wale watakao bainika kuwa na maambukizi.

Akitoa Salamu za Chama, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Sikonge Bi. Anna Chambala ameutaka umma kuendelea kuongoza mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa kuelimisha jamii na kuwalinda vijana dhidi ya kila tabia hatarishi inayoweza kusababisha maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Mhe. Rashid Magope amewashukuru wananchi kwa juhudi zao na uelewa wao juu ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi hata kupelekea maambukizi ya virusi vya Ukimwi kupungua kiasi wilayani Sikonge kama takwimu zinavyo onesha mwaka 2023 maambukizi ni asilimia 1.5 ukilinganisha na takwimu za mwaka uliopita 2022 ambapo maambukizi yalikuwa asilimia 1.7.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Bi. Kalista Maina amewasihi wananchi kuendelea kuwa na hofu ya Mungu na kuendelea kuwa waaminifu kwa wale walio katika ndoa ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Ukimwi nchini.

Akiwasilisha Taarifa ya Siku ya Ukimwi Duniani Bi. Haikael Mjema amesema serikali inaendelea na mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi ikiwa ni pamoja na kusaidia kuunda vikundi 42 vya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi,Kuendelea kutoa elimu ya ufahamu juu ya matumizi ya sahihi ya dawa za kufubaza makali ya virusi vya Ukimwi,Kuunda klabu tano za Watoto wanaoishi na virusi vya Ukimwi,kuendelea kuwa na vituo ishirini na moja vya kutolea dawa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi pamoja na Upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya Virusi vya Ukimwi katika vituo vyote vya kutolea huduma sambamba na upatikanaji wa kondomu (mipira ya kiume) kwa mwaka mzima.

Akihitimisha maadhimisho hayo Mhe. Chacha amewashukuru wadau wote walio mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi na Ukimwi ikiwa ni pamoja na MDH, IDT, CSSC, NACOPHA na COMPASSION Tanzania.


Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa