• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MWENGE WA UHURU WAZINDUA ZAHANATI YA KISASA SIKONGE

Imewekwa: September 4th, 2019

MWENGE WA UHURU WAZINDUA ZAHANATI YA KISASA SIKONGE

Na Evelina Odemba, Sikonge

MBIO za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2019  zimezindua mradi wa Zahanati ya kisasa uliotekelezwa na Serikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora kwa gharama ya zaidi ya Shilingi mil. 261.6 katika kijiji cha Kikungu kata ya Chabutwa.Zahanati hiyo inayotarajia kunufaisha wakazi zaidi ya 7,000 wa kata ya Chabutwa na kata jirani za Ipole na Kipanga ni ya kipekee katika wilaya hiyo kutokana na kutekelezwa kwa kiwango cha hali ya juu.

Mtendaji wa Kijiji Salome ........ akisoma taarifa ya Mradi wa Zahanati hiyo wakati wa Uzinduzi, pembeni ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sikonge Martha Luleka.

Akizindua Zahanati hiyo jana, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Mzee Mkongea Ally alisema kuwa mradi huo ni miongoni mwa miradi mizuri yenye manufaa makubwa kwa wananchi. Aliwataka akinamama wajawazito na wenye watoto wadogo walio chini ya umri wa miaka 5 na jamii kwa ujumla kutumia Zahanati hiyo ipasavyo kwa kuleta watoto wao kliniki na kwenye chanjo ili wapate huduma za afya.

Mkongea alisema kuwa utekelezwaji wa mradi huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya awamu ya tano wa kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa katika halmashauri zote hapa nchini ili kuwezesha wananchi kupata huduma bora za afya. ‘Mama zetu msiende kwa waganga wa kienyeji, mtapoteza maisha yenu na watoto, tumieni ipasavyo zahanati na vituo vya afya vilivyojengwa na Serikali katika maeneo yenu’, alisema. Aliitaka jamii kuendelea kumuunga mkono Rais Dakt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayofanya katika awamu hii ya utawala wake ili aendelee kufanya zaidi kwa manufaa ya wananchi wote wa taifa la Tanzania.

Naye Mkuu wa wilaya ya Sikonge Peres Magiri alibainisha kuwa kufunguliwa kwa zahanati hiyo kutasaidia sana kupunguza vifo vya mama na mtoto na kutoa huduma kwa wakazi zaidi ya 7,000 wa vijiji 5 vya kata hiyo na kata jirani. Katika taarifa yake Mtendaji wa Kijiji hicho Salome............ alisema kuwa ujenzi wa zahanati hiyo umegharimu kiasi cha shilingi mil. 261.6 ambapo Serikali kuu imechangia shilingi mil. 138.6, Halmashauri shilingi mil. 116.9 na wananchi shilingi mil. 6.

Naye Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Peter Nzalalila alisema zahanati hiyo imejengwa kwa ajili ya wananchi, hivyo akawataka wakazi wa vijiji vyote vya kata hiyo na kata jirani kwenda kupata matibabu wakati wowote wanapohitaji huduma.

 xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa