• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI WILAYA YA SIKONGE AMEFANYA KIKAO NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA.

Imewekwa: November 20th, 2024

Msimamizi wa Uchaguzi Wilayaya Sikonge, Ndg. Seleman Pandawe, amekutana na viongozi wa vyama vya siasawilaya ya Sikonge kwa ajili ya kujadili maandalizi ya uchaguzi wa Serikali zaMitaa utakaofanyika tarehe 27 Novemba, 2024. Katika kikao hicho kilichofanyikakatika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri, Ndg. Pandawe amewashukuru viongozihao kwa kuhudhuria na kuwa sehemu ya majadiliano muhimu kwa mustakabali wauchaguzi huo.

Akifungua kikao hicho,Pandawe amewakumbusha viongozi hao juu ya umuhimu wa kuzingatia sheria nakanuni za uchaguzi wakati wa kutekeleza majukumu yao. Amesisitiza kuwa amani nausalama katika mchakato wa uchaguzi yapo mikononi mwao, na hivyo kila kiongozi anajukumu la kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu.

Katika mada inayohusurushwa, Afisa kutoka ofisi ya Takukuru Wilaya ya Sikonge, Ndg. Salum Makina,ametoa tahadhari kali kuhusu vitendo vya rushwa katika uchaguzi. Ameeleza kuwakutoa au kupokea fedha au kitu chochote kwa mpiga kura ili apige kura kwamanufaa fulani au aache kupiga kura ni kinyume cha sheria na inaweza kusababishamadhara makubwa. Amewahimiza viongozi hao kuepuka vitendo vya rushwa kwa nguvu,ili kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa unakuwa huru na haki.

Kwa upande wake, Kamanda waJeshi la Polisi Wilaya ya Sikonge, SSP. Prosper Ngowi, ametoa wito kwa viongoziwa vyama vya siasa kuzingatia sheria na kanuni zinazohusu uchaguzi, na kuepukakutumia sheria mkononi. Amesema kuwa endapo kiongozi atapata changamoto yoyote,basi hatua za kisheria zifuate kwa haraka. “Hupaswi kujichukulia sheriamkononi. Ukikosewa, toa taarifa kituo cha polisi. Tuna dawati la uchaguzi palena tutachukua hatua mara moja,” ameeleza Kamanda Ngowi.

Viongozi wa vyama vya siasawameonesha furaha yao kwa kufanyika kwa kikao hicho, wakieleza kuwakimewajengea uwezo na kuwakumbusha wajibu wao katika kuhakikisha uchaguziunafanyika kwa haki. Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Ndg. Kulwa JumaFundi, amesema, “Kuna maisha baada ya uchaguzi, tufanye kazi kwa uwazi na haki,naamini hakuna atakayegombana na mtu.”

Akifunga kikao hicho, Ndg.Pandawe ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa viongozi hao na amewatakakutokuwa chanzo cha vurugu na taharuki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa,amesisitiza umuhimu wa kufanya uchaguzi katika mazingira ya amani.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa