• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA TABORA AKAGUA MRADI WA UJENZI WA WODI TATU KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA SIKONGE

Imewekwa: April 21st, 2021

MKUU WA MKOA WA TABORA AKAGUA MRADI WA UJENZI WA WODI TATU KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA SIKONGE

Na Anna Kapama

21 Aprili, 2021

Mkuu wa MKOA wa Tabora Dkt.Philemon Sengati amefanya ziara Wilayani Sikonge leo na kukagua mradi wa ujenzi wa majengo matatu ya Hospitali ya Wilaya ya Sikonge ikiwemo Wodi ya kina mama, wanaume na wodi ya wazee na kujiridhisha na maendeleo ya ujenzi huo ambao umeanza mwezi wa nne mwaka 2021.

Aidha, Dkt.Sengati amewapongeza viongozi na wasimamizi  kwa kusimamia vizuri mradi huo.

Pia, Mkuu wa mkoa amempongeza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Sikonge, Tito Luchagula kwa kuwasimamia vyema viongozi na idara zinazohusika katika ujenzi huo akiwapa viapaumbele mafundi  ujenzi wanaopatikana Wilaya ya Sikonge na kuongeza kuwa ni jambo jema kuwapa fursa hizo kwa kuwa itakuza ujuzi na maendeleo binafsi kwa wakazi hao.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewataka watoa huduma za afya Wilayani hapo kuzingatia na kufuata taratibu sheria na kanuni za utoaji wa huduma za afya,huku akisisitiza matumizi ya lugha nzuri  kwa wagonjwa.

Aidha,katika utoaji wa huduma za afya bure kwa watu wenye makundi mbalimbali  wakiwemo wajawazito,wazee na watoto chini ya umri wa miaka mitano, Dkt.Sengati amesema  wapatiwe huduma hizo kwa kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa na kuongeza kuwa wasitozwe gharama yoyote.

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Sikonge, Renatus Mahimbali akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ameishukuru  Serikari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwapatia fedha kwa ajili ya kujenga Hospitali ya Wilaya,huku akimshukuru  Mkuu wa Mkoa kwa kufanya Ziara katika Wilaya hiyo na kuongeza kwamba  uongozi utasimamia vyema miradi yote ya maendeleo.

Mradi huu wa ujenzi wa majengo matatu katika  Hospitali ya Wilaya ya Sikonge utagharimu Shilingi Milioni 500 mpaka kukamilika kwake,na baada ya kukamilika utaongeza ufanisi katika kutoa huduma za Afya na kupunguza vifo visivyo vya lazima Wilayani hapa.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa ameambatana na Katibu Tawala Mkoa, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Mhandisi wa Mkoa, Katibu Tawala Msaidizi Mipango, Mhasibu Mkoa na Waandishi wa Habari.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

    June 14, 2025
  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

    June 06, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa