• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

Imewekwa: May 7th, 2025

Na Edigar Nkilabo


Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi INEC Mhe, Jaji wa Mahakama Kuu Asina A. Omary amefanya ziara Wilayani Sikonge na kukagua mwenendo wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya Pili.

Akizungumza katika ziara hiyo baada ya kutembelea vituo vitatu vya kata za Sikonge na Misheni Mhe.Asina alisema ameridhishwa na huduma wanayopatiwa wananchi wanaofika katika vituo vya kuboresha taarifa katika Daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili.

“Nimeona wapo wanaokuja kujiandikisha kwa mara ya kwanza,wengine wanahama vituo na baadhi yao wanaboresha na kuhakiki taarifa zao wote hawa nimeona wanahudumiwa vizuri na kupata kadi zao kwa wakati, naamini wakati ukifika basi wataenda kutimiza haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi wanaowataka yaani madiwani, wabunge na Rais”alisema.

Naye Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Sikonge Mwl.Benjamin Mshandete alisema zoezi hili limetoa fursa kwa wakazi wote wa Wilaya ya Sikonge wenye sifa ya kupiga kura kwenda kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika vituo vilivyopo na kupata kadi, jambo ambalo ni la kuishukuru Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa kuhakikisha kila mtu anapata haki yake.

“Jimbo letu la Sikonge linavituo 35 ambavyo vinapatikana katika kata zote 20 zilizopo Wilayani Sikonge hivyo kila mwananchi aliyepitwa na zoezi hili awamu ya kwanza safari hii amepata huduma, kwakweli tunaishukuru Serikali na INEC kwa kuwezesha zoezi hili kwa uarahisi”amesema.

Aidha Mwl.Mshandete alisema zoezi limeenda kwa amani na utulivu katika vituo vyote 35, ambapo changamoto pekee zilizojitokeza ni pamoja na kunyesha kwa mvua katika baadhi ya kata ambayo ilichangia kuathiri idadi ya wateja kufika vituoni.

Baadhi ya wananchi kutoka katika vituo tofauti tofauti vya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura walipoulizwa juu ya zoezi hilo walisema huduma zilikuwa zinatolewa kwa weledi na haraka huku wengine wakisema kuwa mashine za Biometriki za sasa zimeboreshwa hazichukui muda mrefu kutoa vitambulisho.

“Yaani nimefika tu sijachukua muda mrefu nimepata huduma na vitambulisho vya safari hii havifutiki haraka  vinaonekana vizuri, kwakweli nitoe wito kwa wengine ambao hawajapata wawahi vituoni”

Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya Pili kwa wilaya ya Sikonge na Mkoa wa Tabora kwa ujumla lilianza Mei, Mosi na kufikia tamati tarehe 07, Mei mwaka huu.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa