• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MAPAMBANO DHIDI YA VVU SIKONGE

Imewekwa: December 2nd, 2018

MAPAMBANO DHIDI YA VVU SIKONGE

Maambukizi  ya Virusi Vya UKIMWI  wilayani Sikonge mkoani Tabora yapungua kutoka asilimia 5.5% mwaka 2017 hadi kufikia asilimia 3.2% mwaka 2018.

Takwimu hizo zilitolewa na mratibu wa UKIMWI ndugu Nicholas Magoha katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambapo wilayani Sikonge yalifanyikia katika kijiji cha Mlogolo na kubeba kaulimbiu  ‘’JIPIME JITAMBUE ISHI”

Pia maadhimisho hayo yaliambatana na uchangiaji damu kwa hiyari ambapo jumla ya wananchi 18 walijitokeza kuchangia damu. Vilevile wananchi 213 ikiwemo wanafunzi wa shule ya msingi, pamoja na wazee walipima ili kujua afya zao, kati yao 3 waligundulika kuwa na VVU.

Katika maadhimisho hayo, mgeni rasmi alikuwa Mhe. Peter Nzalalila Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, alitoa rai kwa sekta ya afya kuongeza vituo vya kuhudumia wagonjwa wa UKIMWI kutoka vituo 15 vilivyopo hadi kufikia vituo 35 ikiwa ni jumla ya vituo vya afya vilivyopo Sikonge.

Vilevile Mhe. Mwenyekiti  alikemea unyanyapaa dhidi ya wagonjwa wa UKIMWI, na kusema ‘’ UKIMWI ni ugonjwa kama magonjwa mengine ni kwanini watumiaji wa ukimwi wamezee dawa chumbani?” aliwataka watumiaji wa dawa za VVU kuwa huru kutumia dawa zao bila kificho.

Aidha Mhe. Nzalalila alisisitiza kuepukana na ngono nzembe kwa kusema ‘’UKIMWI upo na UKIMWI bado tishio hivyo wanachi wajihadhari” na kuwataka wananchi wajiepushe na imani potofu kwa kukimbilia kwa waganga mara tatizo linapotokea. Pia waganga wa kienyeji waepuke kuchanja wagonjwa kwa kutumia wembe mmoja kwani ni chanzo kimoja wapo cha maambukizi  ya ugonjwa hatari wa UKIMWI.

Sanjari na hayo Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge  Bi.  Martha Luleka alisema ‘’ Afya ni mali na kama hauna Afya basi hauna mali.”

Mkurugenzi aliwasisitiza wana sikonge juu ya 90 tatu na kufafanua 90 ya kwanza ni kuhakikisha 90% ya watanzania na dunia nzima wawe wamepima na kujua afya zao ifikapo 2020.  90% ya pili ni waathirika wa ugonjwa UKIMWI wawe wameshaanza kutumia dawa za kupunguza maambukizi  ya VVU na 90% ya tatu ni kuhakikisha waathirika wa UKIMWI waliopima na kuanza kutumia dawa za kupunguza makali wawe na uhakika wa maisha yao. Hivyo kuwataka wananchi wote wa Sikonge kupima na kujua afya zao ili waweze kuzilinda.

Maadhimisho hayo pia yaliambatana na vikundi mbalimbali vya burudani ambavyo vilikuwa na ujumbe uliotoa elimu juu ya ujongwa hatari wa UKIMWI. Pia katika michezo kulikuwa na mpira wa miguu na mpira wa pete ambapo timuya mpira wa miguu  ya Sikonge iliibuka kidedea kwa kuinyuka magoli mawili timu ya Mlogolo.

Wananchi pia walipata nafasi ya kutoa pongezi zao kwa viongozi wilayani Sikonge na uongozi wa serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe. Dkt. Jonh Pombe Magufuli kwa kuipa kipaumbele sekta ya afya  kwa kuongeza vituo vya  Afya wilayani Sikonge na kutoa fedha kiasi cha Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, jambo litakalorahisisha utolewaji wa huduma ya afya.


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA TEHAMA SIKONGE

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa