• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MAMBO YATAKUWA "BAMU BAMU"

Imewekwa: May 1st, 2018

Maadhimisho ya sherehe za MEI MOSI 2018 Wilayani Sikonge yamefanyika katika Kata ya Sikonge eneo la kiwanja kipya cha mpira wa miguu karibu na soko la TASAF ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Bwa. Peres Magiri.

Katika sherehe hizo, Mwaka huu Wilayani Sikonge zimeratibiwa na Chama cha Wafanyakazi TUGHE ambapo ni kawaida ya vyama hivi hapa Wilayani kubadilishana kila Mwaka katika kuratibu zoezi zima la sherehe.

Aidha, sherehe hizo zilianzia katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa maandamano ya wafanyakazi wote pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Mbirani waliotumbuiza kwa nyimbo na ngoma katika msafara kuelekea uwanjani.

Mgeni rasmi alipanda jukwaani kwa ajili ya hotuba baada ya kupokea risala iliyosomwa na muwakilishi kutoka TUGHE Bwa. Gerald Mwagalazi, risala hiyo ilikuwa na malalamiko mbalimbali ya watumishi ikiwemo madai ya likizo za watumishi.

“Awamu hii ya tano ya Rais wetu Mhe. John Pombe Magufu imelenga kuibadilisha Tanzania na dalili zote zinaonesha kuwa mambo yanaenda kuwa bamu bamu” alisema hayo mgeni rasmi.

Aidha, aliwapongeza wafanyakazi kwa namana ya pekee kwa jitihada wanazozifanya katika kuleta maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla. “ Mataifa makubwa yaliyoendelea yamefika hatua hiyo kwa jitihada kubwa za wafanyakazi katika kutimiza wajibu wao, ni imani yangu kuwa wafanyakazi mtasimama imara kuhakikisha mnalitumikia Taifa letu kwa bidii na nguvu zenu zote ili kuhakikisha tunasonga mbele” alisisitiza mgeni rasmi.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Dakt. Simon Ngatunga aliwataka viongozi wa vyama vya wafanyakazi kuwawakilisha ipasavyo wale waliowachagua. “Inashangaza wafanyakazi bora wa Mwaka 2015/2016  hawajalipwa mpaka leo, na leo ninapata taarifa jukwaani kwamba kuna hawa hawakulipwa…nyinyi ni kiunganisho kati ya mimi mwajiri na watumishi hawa, mje tukae chini tutatuwe kero hizo na sasa wale wote nilioletewa majina yao hapa, kesho waje ofisini wachukue pesa zao” alisema Mkurugenzi.

Aidha, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Mhe. Peter Nzalalila alitoa agizo katika sherehe hizo, kuwa robo ya pili ya Mwaka ujao waletewe mkakati wa maandalizi katika kikao cha baraza la Madiwani baada ya kuona maandalizi ya sherehe za Mwaka huu hayakuwa vizuri sana. “Kwa sababu sisi wananchi tunawategemea sana wataalam wetu, pia maendeleo yanategemea wao… Sasa tukionekana kama hatuwaonioni hivi haipendezi” alisema Mwenyekiti huyo.

Sherehe hizo zilihitimishwa kwa kutoa vyeti kwa wafanyakazi bora kutoka katika kila idara na zawadi za fedha ambazo zitaingizwa katika akaunti zao moja kwa moja kupitia mfumo mpya wa malipo wa TISS ambao umeanza kutumika wiki hii.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA TEHAMA

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE WAPIGWA MSASA JUU YA MATUMIZI YA MFUMO WA E-UTENDAJI (PEPMIS)

    June 25, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAPATA HATI INAYORIDHISHA TAARIFA YA UKAGUZI YA MWAKA 2023/2024

    June 14, 2025
  • UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA WAPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO KUTOKA 74% HADI 43% WILAYANI SIKONGE

    June 13, 2025
  • VIJIJI 16 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA UANDAAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

    June 06, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa