• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MAMBO SHWARI KWA KIDATO CHA TANO NA SITA SHULE YA SEKONDARI SIKONGE

Imewekwa: September 22nd, 2025

Na Linah Rwambali


Zaidi ya Shilingi Milioni mia tano zimetolewa na serikali kwaajili ya kuanzisha kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari Sikonge ikiwa ni juhudi za serikali katika kuboresha huduma ya elimu nchini.

Kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa shule Bi Loveness Mwenda shule pesa hizo zilipokelewa mnamo Juni 2024 kwaajili ya mradi wa ujenzi wa mabweni mawili, madarasa mawili, matundu kumi ya vyoo na nyumba ya mwalimu ya mbili kwa moja. .

Mradi huo ulikuja ili kuiwezesha shule kuwa na kidato cha kwanza hadi cha sita sababu awali shule ilikuwa  na kidato cha kwanza hadi cha nne pekee wakati ilipoanza mnamo mwaka 2023.

Bi.Mwenda anasema mradi huo una uwezo wa kuhudumia wanafunzi 180 yaani mabweni mawili, kila moja likiwa na uwezo wa kubeba wanafunzi themanini wakati kwa upande wa madarasa manne kila moja likiwa na uwezo wa kubeba wanafunzi arobaini.

“Hata sasa wanafunzi 12 wa kidato cha tano wameripoti shuleni hapo wavulana kumi na wasichana wawili” anasema.

“Kwa sasa shule inatoa mchepuko mmoja wa HGE (History, Geography, Economics) ambapo kuna walimu wote wanaohusika na kufundisha masomo hayo yote” anasema.

Akizungumzia umuhimu wa mradi huo Bi. Loveness anasema anashukuru serikali kwa ujenzi wa mabweni, madarasa, nyumba ya mwalimu na matundu kumi ya vyoo maana utamkinga kijana na vishawishi na kupata muda mzuri wa kujisomea.

“Mtaani kuna makundi ya wavuta bangi, vibaka na mengineyo. Mtoto anapokaa mazingira ya bwenini inamlinda dhidi ya hayo yote sababu amezungukwa na wanafunzi wenzake ambao wana nia kama yake yaani kusoma na kufaulu”

“Kwa upande wa wasichana wanaepuka vishawishi vya kujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi na hatimaye kupata mimba ambazo hupelekea mwanafunzi kushindwa kutimiza ndoto zake” anasema.

Aliongeza kuwa “watoto wanapoletwa hapa wanajikinga dhidi ya hayo yote sababu huwekwa chini ya mfumo mmoja wa kuwaongoza, wanaelekezwa njia ya kupita na kuwekewa sheria kwa atakayeonekana kukiuka mfumo”.

Aidha Bi Loveness anasema kwa upande wa nyumba ya mwalimu itawezesha wanafunzi kupata msaada iwapo changamoto yoyote itajitokeza.

“Mwalimu kuishi ndani ya shule itawezesha wanafunzi kutoa taarifa iwapo kuna tatizo lolote mfano mtoto kuumwa, umeme kukatika na mengineyo.

“Naishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutoa fedha kwaajili ya utekelezaji wa mradi huo ambao utaleta tija katika sekta ya elimu Wilayani Sikonge na Tanzania kwa ujumla. Hata sasa tumeshapokea wanafunzi 12 wa kidato cha tano ambao walianza kusoma mnamo Mnamo Julai mwaka huu wakiwemo wavulana kumi na wasichana wawili japo mradi una uwezo wa kupokea wanafunzi 160 yaani madarasa manne ambapo kila darasa linachukua wanafunzi arobaini na mabweni mawili, kila bweni lina uwezo wa kubeba wanafunzi themanini.

Mbali na Mwalimu huyo nao baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha tano katika shule hiyo, wameelezea namna wanavyonufaika na mradi huo kwa mfano Justine Richard anasema mabweni ni mazingira stahiki kwao katika kujisomea kwasababu kuna umeme, huduma ambayo inawawesha kujisomea nyakati za usiku.

“Baadhi ya wanafunzi hatuna umeme majumbani kwetu, kuishi shuleni kunatuwezesha kujisomea katika muda wowote tunaohitaji” anasema.

“Unapokua nyumbani unalazimika kujisomea wakati wa mchana tu wakati wengi tunapendelea kujisomea usiku sababu ni muda uliotulia, unaposoma muda huo unaelewa mambo kirahisi sababu ya uwepo wa utulivu katika muda huo.Naishukuru serikali kwasababu wametutengenezea mazingira ambayo yatatuwezesha kupata muda mwingi wa kurejea yale tuliofundishwa darasani kitu ambacho tusingeweza kukipata tukiwa tunajisomea nyumbani” anasema.

Fatma Juma anasema  muda ambao angeupoteza katika kusafiri umbali mrefu wakati anaenda na kurudi shuleni sasa atautumia katika kujisomea kwa bidii akiwa bwenini.

“Kuishi bwenini kunaniwezesha kuokoa muda ambao ningeupoteza wakati wa kwenda na kurudi shuleni. Ninategemea kufanya vizuri katika masomo yangu maana kuishi shuleni kunaniwezesha kusoma kwa kadri nitakavohitaji” anasema.

“Najisikia furaha kupata fursa ya kusoma katika shule hii mpya yenye vifaa na walimu wa kutosha jambo ambalo litachangia kutuwezesha wanafunzi kupata matokeo mazuri” anasema.

Naye Nassoro Kulwa anasema kuwa anafurahi kuishi katika shule ya bweni kwa mara ya kwanza na kupata uzoefu wa kuwa karibu na walimu ambao wanaishi katika nyumba ya mwalimu ilyopo jirani nao.

“Ujenzi wa mabweni na nyumba ya mwalimu umetuwezesha kujenga ukaribu wa kielimu na kijamii na walimu wetu sababu tunaishi karibu na nyumba ya mwalimu. Ninapokua najisomea na kushindwa kuelewa mahali fulani, naweza kumfata mwalimu nyumbani kwake na ukaribu huo wa kuulizana changamoto za kielimu huzalisha urafiki kati ya mwalimu na mwanafunzi jambo ambalo humfanya mwanafunzi kuwa huru kumshirikisha mwalimu hata katika changamoto zake zingine za kijamii” anasema.

Matangazo

  • TANGAZO LA FURSA ZA UWEKEZAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE September 10, 2025
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA SIKONGE SEKONDARI KUANZA KUFUNDISHWA TEHAMA KWA VITENDO

    November 25, 2025
  • WANAFUNZI WA KIKE WILAYANI SIKONGE WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

    November 23, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE AHIMIZA UWAJIBIKAJI

    November 20, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA AFYA TARAFA YA KIWERE

    November 17, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Matangazo
  • Zabuni
  • Matukio
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa