• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MADIWANI WASHUSHA NYUNDO KWA WAHUDUMU WA AFYA SIKONGE

Imewekwa: May 23rd, 2019

MADIWANI WASHUSHA NYUNDO KWA WAHUDUMU WA AFYA SIKONGE.

Wahudumu wa Afya Wilayani Sikonge waagizwa kuwa makini katika kutoa huduma kwa jamii inayowazunguka.

Agizo hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Sikonge Mhe. Peter Nzalalila katika baraza la Madiwani  lililofanyika mapema jana kwenye ukumbi wa chuo cha ufundi kilichopo Sikonge, baada ya madiwani kutoa malalamiko ya wananchi kwa baadhi ya wahudumu wa Afya kutowatendea haki wagonjwa wanapofika katika vituo vya kutolea  huduma hiyo.

Aidha, Mhe. Nzalalila alitoa onyo kali kwa watoa huduma za afya kuzingatia utaratibu wa kuwahudumia wagonjwa kwa upendo kwani ndivyo maadili yanavyowataka na waache kuwa na fikra za kuzani kuwa maelekezo wanayopewa ni siasa tu kwa sababu  swala la Afya ni swala nyeti sana na ndio maana serikali imetoa pesa nyingi kuhudumia sekta hiyo.

“juzi tu serikali imeidhinisha fedha nyingi kwa ajili ya dawa na huduma za Afya, lakini leo mgonjwa anafika hospitali anaambiwa kuwa hakuna dawa. Lugha hii ikome kwasababu hatutovumilia habari hii katika Wilaya yetu” alisema.

Hoja hii iliibuka baada ya Mhe. Upendo Mgombozi diwani Kata ya Kipanga kueleza namna ambavyo mwananchi wake aliyekuwa mjamzito kutopatiwa huduma stahiki huku akiambiwa kwenda kununua dawa katika zahanati ya jirani

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge wakifatilia kwa makini mjadala unaoendelea kwenye vikao vya baraza.

Wajumbe walienda mbali zaidi na kuongeza kuwa kumekuwa na matukio mbalimbali ya wanawake wajawazito kufika katika vituo vya kutolea huduma za afya na kurudishwa nyumbani kwa kigezo cha kuwa muda wao wa kujifungua haujafika, kitendo hiko kimepelekea baadhi ya wajawazito kujifungulia njiani.

Akikemea kitendo hicho Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Peres Magiri alisema kuwa yeyote atakayebainika kufanya vitendo hivyo hatovumiliwa atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. “tuliwahi kumuweka ndani muhudumu wa Afya hapa hapa Sikonge kwa vitendo hivyo , sitovumilia kuona mambo haya yanajirudia tena”.

Akijibu tuhuma hizo kaimu mganga mkuu wa Wilaya Theopista Elisa alisema kuwa kitaalamu hutokea mjamzito akawahi kujifungua tofauti na muda uliooneshwa kwenye vipimo ambapo hali hiyo ikitokea nesi anaweza kutumia majibu ya vipimo kumruhusu mama kurudi nyumbani hali hii inachangia kuwa sababu ya baadhi ya  matukio kama hayo yakatokea.

Vile vile Dkt Theopista alihakikishia baraza kuwa anafanyia kazi jambo hilo na matukio yote ya unyanyapaa wa wagonjwa unaofanywa na watoa huduma wa afya ili kuzuia matukio kama hayo yasiweze kujitokeze tena Wilayani hapa huku akiwaomba madiwani na wananchi wote kutoa ushirikiano kwa kuwabainisha wale wote wanaohusika na malalamiko hayo ili hatua za kinidhamu ziweze kuchukuliwa zidi yao.

Sanjari na jambo hilo pia baraza hilo pia walizungumzia mambo mbalimbali ikiwemo ukarabati wa miundombinu ya barabara inayofanywa na Wakala wa Barabara vijijini na mjini TARURA ambapo kwa Sikonge imeonekana kufanya vizuri.

`             IMEANDALIWA NA 

KITENGO CHA TEKINOLOJIA HABARI NA MAWASILIANO TEHAMA

SIKONGE.


Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SIKONGE YAADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO KWA KUFANYA USAFI

    April 26, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa