• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MADIWANI WALIOPITA BILA KUPINGWA WAAPISHWA RASMI

Imewekwa: July 3rd, 2019

SIKONGE- MADIWANI WALIOPITA BILA KUPINGWA WAAPISHWA RASMI

Hakimu Wilayani Sikonge Mhe. Amando Nyami amewaapisha Madiwani hao wateule waliopita bila kupingwa katika uchaguzi mdogo mapema mwezi Juni 2019.

Madiwani hao ni Mhe. John Mbogo wa kata ya Ipole na Mhe. Josephine Mayanga wa kata ya Pangale wote kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliapishwa katika ukumbi wa chuo cha ufundi (FDC) mbele ya wajumbe wa kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, wataalamu wa Halmashauri, viongozi wa Chama Tawala CCM pamoja na Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge.

Madiwani hao walipita bila kupingwa kufuatia wagombea wengine kutoka vyama pinzani kujitoa kwa hiari kushiriki uchaguzi baada ya kusema kuwa wanaimani na viongozi hao waliotokana na chama Tawala kuwa wataongoza vyema.

Aidha wakati wa kuapishwa kwa Madiwani hao Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Sikonge, Marha Luleka alitoa pongezi zake kwa viongozi hao wapya  huku akiahidi kufanya nao kazi kwa ushirikiano mkubwa.

Akizungumzaa kwa niaba ya chama, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Mhe. Anna Chambala alitoa nasaha zake kwa wateule hao kuhakikisha kuwa wanatekeleza vyema ilani ya uchaguzi ya  CCM kwa kuwatumikia wananchi wote bila kuwabagua kutokana na itikadi zao.

Wahe. Madiwani Wapya Wakiwa kwenye Picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri (waliokaa) pamoja na Whe. Madiwani kamati ya fedha mara baada ya kuapishwa mapema leo hii.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Sikonge Mhe. Peter Nzalalila aliwapokea kwa mikono miwili Madiwani hao huku akiwataka kuondoa woga wa kuchangia mawazo ya kimaendeleo kwani lengo ni kuwawakilisha vyema wananchi hususani katika swala la maendeleo, kwa kuzingatia kanuni na taratibu zinazowaongoza madiwani. Ili kusisitiza hilo Mhe. Nzalalila aliwakabidhi vitabu vya kanuni za Madiwani ili viwape muongozo sahihi.

Tume ya Uchaguzi ilitoa kibali cha kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa kata ya Ipole baada ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo kupitia tiketi ya CHADEMA kujivua uwanachama na madaraka na kujiunga rasmi CCM ili kuonesha kuwa anakubaliana na utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM sanjari na kuunga mkono utendaji kazi wa Mhe. John Pombe Magufuli Rais wa Tanzania.

Wakati Diwani wa Kata ya Pangale Mhe. Josephine ameingia madarakani baada ya aliyekuwa Diwani wa Kata hiyo kufikwa na Mauti. Hivyo uchaguzi ulitangazwa na baada ya kukosekana upinzani mteule huyo alipitishwa bila kupingwa na leo hii wameapishwa rasmi tayari kuanza majukumu yao.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

TEHAMA SIKONGE

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa