• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Sikonge District Council
Sikonge District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • Idadi ya Watu
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya Viongozi
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Mifugo na uvuvi
      • Afya na Ustawi wa jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira na Taka ngumu
      • Kilimo, Umwagilaji na Ushirika
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Uchimbaji wa Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo Ndogo
    • Miongozo Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya sanaa
      • Sanaa za picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Habari mpya
    • Matukio

MAADHIMISHO YA TB WILAYANI SIKONGE

Imewekwa: March 25th, 2018

Maadhimisho ya Siku ya Kifua Kikuu (TB) Duniani yamefanyika jana Kimkoa katika Kata ya Kitunda maeneo ya Mgodini Wilayani Sikonge ambapo Mgeni Rasmi akiwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Mhe. Peter Nzalalila.

Mratibu wa TB Mkoa wa Tabora, Benedict Komba alitoa historia ya maadhimishi hayo kuwa yalianza mwaka 1882 baada ya kugundulika kwa vimelea vya ugonjwa wa TB, ndipo ikawa siku ya maadhimisho ya ugonjwa wa TB Duniani kote. Pia alieleza kuhusu Kauli mbiu ya Mwaka huu kuwa, Viongozituwe mstari wa mbele kupambana ili kutokomeza Kifua Kikuu. Mratibu huyo alieleza kuwa takwimu zinasema kwa kila kundi la watu Laki Moja kuna wagonjwa 327 wa Kifua kikuu, hivyo ugonjwa huu ni hatari sana.

Nae mratibu wa TB Wilaya ya Sikonge, Dr. Buswelu alitoa taarifa ya zoezi zima la upimaji ambapo watu zaidi ya 753 walikuwa wamepima HIV na watu 134 walikuwa wamepima TB na 6 kati yao walibainika kuwa na vimelea vya TB, hivyo walianza kupata tiba. Mpaka zoezi linaisha watu 922 walikuwa wamepima HIV, 17 kati yao walikuwa na Virusi na kwa upande wa TB watu 196 walichunguzwa, 7 kati yao walikuwa na TB.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya, Venance Ngeleuya aliwaeleza wananchi kuwa wanapoona dalili zinazoendana na ugonjwa wa TB, wafike haraka katika vituo vinavyotoa huduma ya TB. " Msiogope kwenda kupima kwa kuwa baadhi ya dalili za TB zinafanana na dalili za UKIMWI basi mtu unafikiri ni UKIMWI bila hata kupima...," alisema Kaimu huyo.

Aidha, mgeni rasmi alitoa agizo la kuanzisha huduma ya vipimo na tiba ya TB katika Zahanati ili kupeleka huduma karibu na wananchi. Alisema hayo baada ya kuona kuwa huduma hiyo inatolewa katika Vituo vinne tu Wilaya nzima. " Naagiza kuanzia Mwezi ujao vituo nane vianze kutoa huduma hiyo huku Mganga Mkuu Wilaya anaandaa utaratibu ili Zahanati ikiwezekana zote ziwe zinatoa huduma hiyo," alisema mgeni rasmi.

Pia, mgeni rasmi alisema kuwa eneo la mgodi wa Kitunda linawatu wengi sana wanaotoka sehemu mbalimbali lakini huduma ya matibabu iko mbali sana. Aliwaita mbele viongozi wa wachimbaji madini na Mtendaji wa Kata hiyo kisha akasema, "wiki ijayo mniletee mpango mkakati wa kuanza ujenzi wa Zahanati katika mgodi huu na wananchi hapa wako tayari kwa hilo, au sio jamani!?" wananchi walifurahi na kusema wako tayari kwa hilo. " Mtendaji hiki ni kipimo chako cha kuendelea kuwepo hapa Kitunda, vinginevyo Nyahua itakuhusu" alisema Mhe. Nzalalila.

Baada ya Mtendaji huyo kuambiwa kuwa atahamishiwa Kata ya Nyahua endapo atashindwa kufanikisha ujenzi wa Zahanati mgodini, mgeni rasmi alitembelea mabanda yaliyokuwa yanatoa huduma ya vipimo na kuridhishwa na zoezi hilo.

Kabla ya kuanza maadhimisho, Mwenyekiti alipata fursa ya kutembelea mradi wa Ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto, Maabara na Nyumba ya Mganga katika Kituo cha Afya Kitunda. Wodi hiyo ipo katika hatua ya Msingi, nyumba ya Mganga ipo hatua ya lenta na Maabara msingi umekamilika.

Aidha, Mkandarasi anaesimamia ujenzi huo aliahidi kuwa mpaka kufikia tarehe 30 Mei 2018 ujenzi utakuwa umekamilika kwa Majengo yote matatu (3). Akizungumza Mhandisi huyo alisema,

" Changamoto kubwa iliyotupata ni kubadilika kwa mchoro wa ramani ya jengo la wodi ya mama na mtoto wakati ambapo ujenzi ulikuwa umeshaanza."

Mwenyekiti Nzalalila alichukizwa sana na gharama kubwa anayolipwa fundi huyo na kusema, " hii sio maana halisi ya 'Force Account', kwa sababu gharama ni kubwa mno, zaidi ya Milioni 10 kwa jengo moja analipwa ' local' fundi." Baada ya kusema hayo alitoa agizo kwa Viongozi na wataalam kuwa jambo kama hilo lisijirudie tena katika Halmashauri hii.

Matangazo

  • TANGAZO LA ZABUNI YA KUKODISHA CANTEEN [MGAHAWA] MPYA KWENYE JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZAABUNI YA KUMPATA MWEKEZAJI KATIKA KIWANDA CHA KATI CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI(MARUDIO) June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA USAFI KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI June 07, 2023
  • ZABUNI YA KUTOA HUDUMA YA ULINZI June 07, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI KININGA - KATA YA IPOLE

    May 09, 2025
  • MJUMBE WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WILAYANI SIKONGE

    May 07, 2025
  • KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE WILAYANI SIKONGE

    April 29, 2025
  • WATENDAJI WA INEC WILAYANI SIKONGE WAMEKULA KIAPO CHA UADILIFU, KUJIWEKA KANDO NA VYAMA VYA SIASA.

    April 29, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Wilayani Rungwe - Mbeya.
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Mkoa wa Tabora
  • TAMISEMI
  • Urambo DC
  • UTUMISHI
  • Kaliua DC

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Sikonge DC

    Anuani ya Posta: S.L.P 70 Sikonge, Tabora

    Simu: 0767135460

    Simu: 0767135460

    Barua pepe: ded@sikongedc.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma zetu

Hatimiliki ©2017Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Haki zote zimehifadhiwa